Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
 MKUU wa Wilaya ya Temeke  Mh. Felix Lyaniva akishirikiana na wafanyakazi wa Benki wa KCB pamoja na   wafanyabiashara wa eneo la Mbagala Zakhiem wamefanya  usafi kwa pamoja katika eneo hilo ikiwa ni kuweka mazingira safi na salama.

Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mh. Felix Lyaniva ameiomba Benki ya KCB  kutoa huduma nzuri na bora kwa wakazi wa Mbagala, na ikiwezekana kuwapa punguzo la riba na masharti nafuu katika mikopo ili kuweza kupata wateja wengi zaidi.


Ameyasema hayo mapema wakati akifungua zoezi la usafi katika wilaya hiyo lililofanywa na benki ya KCB maeneo ya Mbagala Zakhiem, na kuwaomba watoe mikopo ya riba nafuu katika eneo hilo kwa kuwa lina wafanyabiashara wengi na wadogo wakiwa wanahitaji kupewa nguvu ili waweze kufikia malengo yao.



Lyaniva ambaye alikuwa Mgeni Rasmi, aliipongeza Benki ya KCB kwa juhudi na kufanikisha kuwaleta wadau mbali mbali pamoja na wananchi wa Mbagala kushiriki katika kufanya usafi. “Mlichokifanikisha leo si kidogo na ninawapongeza lakini pia iwe chachu ya kutaka kufanya zaidi katika jamii yenu, ni mfano mzuri wa kuigwa hata na makampui mengine.” aliongeza DC Lyaniva.

Aliendelea kusema kuwa anafurahia kuona wawekezaji wengi wanaendelea kuwekeza katika wilaya ya Temeke kwani anategemea ubora wa huduma kwa wananchi wake, lakini pia watamsaidia katika shughuli nyingi za kijamii ikiwemo kujenga Madarasa, Zahanati na hata huduma za usafi katika maeneo hayo kwani ndio malengo ya serikali ya awamu ya tano.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke  Mh. Felix Lyaniva  akiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya KCB Zuhura Muro(kulia)  wakifanya usafi na pamoja kwa ajili ya kuweka mazingira safi na salama Mbagala Zakhiem Jijini Dar es salaam.
Wafanyakazi wa  Benki ya KCB, wafanyabiashara wadogo wadogo, kampuni ya Green Waste wakiendelea na usafi Mbagala Zakhiem kwa ajili ya kuweka mazingira safi na salama.
Picha ya Pamoja

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...