Na Mwandishi wetu
MRADI mpya wa utafiti na wa kujenga uwezo wa kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kutoa ushauri wa kisera katika nyanja za kilimo na mfumo wa chakula nchini Tanzania umezinduliwa jana.
Akizindua mradi huo ofisi za Taasisi ya tafiti za kiuchumi na kijamii –ESRF, Waziri wa Kilimo Dk. Charles Tizeba  alisema mradi huo unakuja wakati muhimu ambapo taifa linajikita katika kuelekea uchumi wa kati unaotegemea kilimo.
“Sekta ya kilimo imeendelea kuwa ni Sekta muhimu katika maendeleo ya uchumi wa wananchi na Taifa kwa ujumla hususan katika wakati huu Tanzania inapojizatiti kuelekea uchumi wa viwanda,” alisema Waziri Tizeba huku akisema kwamba sekta ya Kilimo iimekuwa ikiendelea kukua kwa kuchangia asilimia 30 ya fedha za kigeni na kuchangia malighafi za viwanda kwa asilimia 65.
Mradi huo umezinduliwa takaribani miezi mitatu baada ya wizara kuzindua rasmi Program ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo awamu ya pili (ASDP II), yenye lengo la kuleta mageuzi ya Sekta ya kilimo (kilimo, mifugo na uvuvi) ili kuongeza uzalishaji na tija na kufanya kilimo kiwe cha kibiashara zaidi na kuongeza pato la wakulima wadogo.
Pamoja na kufanya uzinduzi huo aliipongeza ESRF na timu nzima ya mradi wa GCRF-AFRICAP kwa kuchangia maendeleo ya sekta ya kilimo kupitia tafiti na kujenga uwezo kwa lengo la kupunguza madhara ya mabadiliko ya tabia nchi kwa makundi ya jamii yaliyokua kwenye hatari zaidi.
Alisema Wizara yake itaendelea kukuza na kulinda maendeleo ya sekta ya kilimo yaliyo endelevu, kwa kuongeza uzalishaji, kuboresha mifumo ya kilimo inayokwenda sambamba na mabadiliko ya tabia nchi.
“Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inazingatia tatizo la mabadiliko ya tabia ya nchi kwa umakini mkubwa sana, na Tanzania ni miongoni mwa nchi chache Barani Afrika ambazo zimefanikiwa kuendeleza Mpango Mkakati wa Kupambana na Mabadiliko ya Tabia ya Nchi,  ili kwenda sambamba na dira ya maendeleo ya taifa 2025.” Alisema Dk. Tizeba.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dk. Tausi Kida akitoa neno la ukaribisho kwa mgeni rasmi Waziri wa Kilimo Dk. Charles Tizeba (hayupo pichani) na washiriki wakati wa hafla ya uzinduzi wa mradi mpya wa utafiti na wa kujenga uwezo wa kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kutoa ushauri wa kisera katika nyanja za kilimo na mfumo wa chakula nchini Tanzania uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF) jijini Dar es Salaam.
 Mgeni rasmi Waziri wa Kilimo Dk. Charles Tizeba akitoa hotuba kabla ya kuzinduzi wa mradi mpya wa utafiti na wa kujenga uwezo wa kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kutoa ushauri wa kisera katika nyanja za kilimo na mfumo wa chakula nchini Tanzania uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF) jijini Dar es Salaam.
 Mgeni rasmi Waziri wa Kilimo Dk. Charles Tizeba (katikati) akizundua rasmi mradi mpya wa utafiti na wa kujenga uwezo wa kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kutoa ushauri wa kisera katika nyanja za kilimo na mfumo wa chakula nchini Tanzania uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF) jijini Dar es Salaam huku Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dk. Tausi Kida (wa pili kushoto), Msimamizi wa mradi wa AFRICAP kwa Tanzania na Mkuu wa Idara ya Ushauri Elekezi –ESRF, Bi. Vivian Kazi (kushoto), Mwakilishi wa, FANRPAN – AFRICAP anayeshughulikia sera (kikanda), Bi. Sithembile Ndema Mwamakamba (wa pili kulia) pamoja na Dr. Susanna Sally (kulia) kutoka Chuo Kikuu cha Leeds nchini Uingereza wakishuhudia tukio hilo.
 Dr. Susanna Sally kutoka Chuo Kikuu cha Leeds nchini Uingereza akiwasilisha mada kuhusu mfumo wa kilimo cha kisasa kincahozingatia mabadiliko ya hali ya hewa wakati wa hafla ya uzinduzi wa mradi mpya wa utafiti na wa kujenga uwezo wa kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kutoa ushauri wa kisera katika nyanja za kilimo na mfumo wa chakula nchini Tanzania uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF) jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Huduma za Utafiti na Matumizi ya taarifa za hali ya hewa TMA kutoka Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Dkt. Ladislaus Chang'a akitoa maoni wakati wa hafla ya uzinduzi wa mradi mpya wa utafiti na wa kujenga uwezo wa kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kutoa ushauri wa kisera katika nyanja za kilimo na mfumo wa chakula nchini Tanzania uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF) jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wadau wa sekta ya kilimo kutoka, vyuo vikuu, taasisi mbalimbali za serikali pamoja sekta binafsi walioshiriki hafla ya uzinduzi wa mradi mpya wa utafiti na wa kujenga uwezo wa kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kutoa ushauri wa kisera katika nyanja za kilimo na mfumo wa chakula nchini Tanzania uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF) jijini Dar es Salaam.
Mgeni rasmi Waziri wa Kilimo Dk. Charles Tizeba akiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa mradi mpya wa utafiti na wa kujenga uwezo wa kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kutoa ushauri wa kisera katika nyanja za kilimo na mfumo wa chakula nchini Tanzania uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF) jijini Dar es Salaam.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...