MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella amewaonya wananchi wa Kijiji cha Kwakibuyu kata ya Kipumbwi wilayani Pangani wanaojishughulisha na uingizwaji wa dawa za kulevya ,wahamiaji haramu na biashara za magendokuacha mara moja vitendo hivyo kabla hawajakumbana na mkono wa sheria huku akiwataka wananchi kuwafichua watu hao.
Eneo la Kipumbwi limekuwa likitajwa kuwa ni miongoni mwa maeneo ambayo kumekuwa bandari bubu ambayo imekuwa ikitumika kwenye matumizi mbalimbali ikiwemo kuingiza bidhaa za magendo, wahamiaji haramu jambo ambalo alisema linapaswa kukomeshwa.
Shigella aliyasema hayo jana wakati wa ziara yake ya kutembelea miradi mbalimbali ikiwemo kuzungumza na wananchi kwenye mikutano ya hadhara wilayani Pangani ambapo alisema Bandari hiyo bubu zimekuwa tatizo kwenye kutumika kwenye matumizi ambayo yasiyokuwa salama.
“Hapa Kipumbwi mmekuwa na tatizo kubwa la bandari bubu ambayo imekuwa kutumika kwenye matumizi yasiyosalama biashara haramu ya kupitisha wahamiaji, dawa za kulevya ama kusafirisha wahamiaji haramu lakini wapo baadhi yenu wanadhamira njema ya kuleta bidhaa kutoka maeneo mengine ikiwemo mkoani Tanga wakati mwengine kivuko kikiwa kimefungwa.
MKUU
wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella akizungumza na wananchi wa Kijiji cha
Kwakibuyu Kata ya Kipumbwi wilayani Pangani wakati wa ziara yake ambapo
aliwataka kuacha kushiriki kwenye vitendo vya biashara haramu za
magendo na uingizaji wa dawa za kulevya.
Katibu Tawala wa wilaya ya Pangani (DAS) Mwl Hassani Nyange akizungumza katika ziara hiyo.
MKUU
wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella katikati akimsikiliza Mkuu wa wilaya
ya Pangani Zainabu Issa wakati wa ziara yake wilayani humo kushoto ni
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji na Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM)
Jumaa Aweso.
Sehemu ya umati wa wananchi wakimsikilizaa Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...