Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Godfrey Ndalahwa, akizungumza wakati wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Jumuiya ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa mjini Dodoma hivi karibuni. Katika maelezo yake mkurugenzi huyo alisema DCB ilidhamini mkutano huo wakiwa kama wadau wakubwa wa serikali za mitaa hii ikitokana na benki hiyo kuanzishwa na manispaa za Jiji la Dar es Salaam na pia kupata fursa ya kuwajulisha manispaa nyingine na wananchi kuwa benki hiyo ilianzishwa kwa lengo la kuwasaidia wananchi hasa wenye kipato cha chini.
: Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Benki ya Biashara ya DCB, Rahma Ngassa akisalimiana na Mkuu wa Kitengo cha Utawala Bora na Ushirikishwaji wa Wananchi Mradi wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta za Umma, Dk Peter Kilima (kushoto), wakati wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Jumuiya ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa mjini Dodoma hivi karibuni. Katika mkutano huo Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Godfrey Ndalahwa (wa pili kushoto) alisema benki hiyo ilidhamini mkutano huo wakiwa kama wadau wakubwa wa serikali za mitaa hii ikitokana na DCB kuanzishwa na manispaa za Jiji la Dar es Salaam na pia kupata fursa ya kuwajulisha manispaa nyingine na wananchi kuwa benki hiyo ilianzishwa kwa lengo la kuwasaidia wananchi hasa wenye kipato cha chini. Kulia ni Meneja wa DCB Dodoma Joseph Njile
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Godfrey Ndalahwa (wa pili kushoto), akiwa na baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo wakati wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Jumuiya ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa mjini Dodoma hivi karibuni. Katika mkutano huo mkurugenzi huyo alisema benki hiyo ilidhamini mkutano huo wakiwa kama wadau wakubwa wa serikali za mitaa hii ikitokana na DCB kuanzishwa na manispaa za Jiji la Dar es Salaam na pia kupata fursa ya kuwajulisha manispaa nyingine na wananchi kuwa benki hiyo ilianzishwa kwa lengo la kuwasaidia wananchi hasa wenye kipato cha chini
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...