NAIBU Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye amefanya ziara ya kukagua upatikanaji wa mawasiliano kwenye Wilaya ya Mkuranga iliyopo mkoa wa Pwani na kuahidi wananchi kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaongeza mawasiliano kwenye Wilaya hiyo ambayo ina viwanda vingi vyenye uwekezaji wa aina mbali mbali

Amesema kuwa katika ziara yake amebaini kuwa yapo baadhi ya maeneo ambayo yanahitaji kuongezewa nguvu ili mawasiliano yaweze kufika eneo kubwa zaidi na kupeleka mawasiliano kwenye baadhi ya maeneo ambayo yana ukosefu wa mawasiliano kwenye Wilaya hiyo kwa kuwa mawasiliano ni maendeleo, uchumi na ulinzi na usalama.

Amefafanua kuwa, “kimsingi mawasiliano yapo Mkuranga ila tunatakiwa kuongeza nguvu ili wananchi wapate mawasiliano. Tunahitaji wananchi wa Tanzania wawasiliane,” amesema Nditiye. Ameongeza kuwa minara iliyopo inaweza kuongezwa nguvu, kampuni nyingine zitafunga mawasiliano kwenye minara ya kampuni nyingine zilizopo na kujenga minara kwenye maeneo ambayo hayana mawasiliano kabisa. 

Nditiye amemshukuru Ulega na kuwapongeza wananchi wa Tanzania kwa kuonyesha uhitaji wa mawasiliano na wamegundua mawasiliano ni maendeleo yao, uchumi, ulinzi na usalama. Amesema kuwa karibu asilimia 60 ya eneo la Mkuranga halina mawasiliano na ameyataka makampuni ya simu yaliyojenga minara kwenye Wilaya ya Mkuranga kuongeza nguvu ya mawasiliano kutoka teknolojia ya 2G hadi teknolojia ya 4G. 
Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye (wa pili kushoto) akifafanua jambo wakati wa ziara yake ya kukagua upatikanaji wa mawasiliano kwenye vijiji mbali mbali vya Wilaya ya Mkuranga. (wa kwanza kushoto) Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi na Mbunge wa jimbo hilo,Abdallah Ulega.
(Picha na Emmanuel Massaka wa Global ya jamii)
Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye (wa kushoto pili ) akimsikiliza kwa makini Mbunge wa Mkuranga Abdallah Ulega kuhusu ukosefu wa mawasiliano ya uhakika kwenye eneo hilo. Wa kwanza kushoto ni Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote Mhandisi Peter Ulanga.
Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta,Nditiye akitoa maelekezo namna minala ya mawasiliano itakavyo jengwa katika ya  Wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...