Waziri wa Kilimo Dkt Charles Tizeba (Mb), akisisitiza mpango wa serikali kukabiliana na njaa wakati akihutubia wananchi waliojitokeza kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya Chakula Duniani Kitaifa ambayo yamefanyika kwenye viwanja vya JK Nyerere katika Halmashauri ya Mji wa Tunduma jana tarehe 16 Octoba 2018. (Picha Na Mathias Canal, WK)
Waziri wa Kilimo Dkt Charles Tizeba (Mb), akikagua banda la Bima ya mazao wakati wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Chakula Duniani Kitaifa ambayo yamefanyika kwenye viwanja vya JK Nyerere katika Halmashauri ya Mji wa Tunduma jana tarehe 16 Octoba 2018.

Na Mathias Canal-WK, Tunduma-Mbeya
KATIKA kukabiliana na upungufu wa chakula unaoweza kujitokeza pindi nchi itakapokuwa kwenye majanga, Serikali imetoa jumla ya shilingi Billioni 15.0 za Kitanzania kwa ajili ya ununuzi wa mahindi kupitia Wakala wa Taifa wa Hifadhi Chakula (NFRA) katika mwaka wa fedha 2018/2019. 

Tayari Wakala wa Taifa wa Hifadhi Chakula (NFRA) umeanza msimu wa ununuzi tangu mwezi Agosti 2018 ambapo nafaka wanayonunua ni kutoka kwa wakulima na vikundi vya wakulima kote nchini. 

Waziri wa Kilimo Dkt Charles Tizeba (Mb), amebainisha hayo jana tarehe 16 Octoba 2018 wakati akihutubia wananchi waliojitokeza kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya Chakula Duniani Kitaifa ambayo yamefanyika kwenye viwanja vya JK Nyerere katika Halmashauri ya Mji wa Tunduma.

Vilevile, NFRA inaendelea kuboresha uwezo wake wa kuhifadhi nafaka kwa kuimarisha kanda zake kupitia mradi wa ujenzi wa vihenge na maghala ya kisasa ili Kuongeza uwezo wa kuhifadhi nafaka. 

Dkt Tizeba alisema kuwa Kupitia mradi huo miundo mbinu ya kisasa ya hifadhi ya chakula zikiwemo maghala na vihenge vya kisasa vinajengwa katika Halmashauri za Wilaya za Babati (Tani 40,000), Mpanda (Tani 25,000) , Sumbawanga (Tani 40,000), Mbozi (Tani 20,000), Songea (Tani 50,000), Shinyanga (Tani 35,000), Dodoma (Tani 20,000) na Makambako (Tani 30,000). 

Alisema, Hifadhi hizo zitatumia teknolojia ya kisasa ya kuhifadhi mazao na hivyo kupunguza upotevu wa mazao ghalani kwa kiasi kikubwa. 

Aliongeza kuwa, Kukamilika kwa mradi huo kutawezesha NFRA kuongeza uwezo wake wa kuhifadhi nafaka kutoka Tani 251,000 hadi kufikia Tani 501,000 ifikapo mwaka 2019/2020.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...