Mchezo wa kufuzu Mataifa Afrika (AFCON) 2019 nchini Cameroon baina ya Tmu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' na Cape Verde umemalizika katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam kwa wenyeji kutoka kidedea kwa mabao 2-0.
Taifa Stars wameshinda magoli mawili yaliyofungwa na mshambuliaji wa Difaa El Jadida ya Morocco Saimon Msuva katika dakika ya 29 akipokea pasi ya Mshambuliaji wa GRC Genk Mbwana Samatta. Mpaka Mapumziko Taifa Stars wanatoka kifua mbele kwa goli 1-0.
Katika kipindi cha Pili, Samatta aliipatia Taifa Stars goli la pili akimalizia pasi ya Mudathiri Yahya, akifuta lawama baada ya kukosa penati katika kipindi cha kwanza.
Taifa Stars walifanya mabadiliko ya kumtoa Abdi Banda na kuingia John Bocco, Mudathir nafasi yake ikichukuliwa na Feisal Toto
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...