Ukosefu wa uwazi na uwajibikaji katika  shughuli za Asasi za Kiraia Tanzania  unaathiri uwezo wa nchi kutambua kiwango cha michango na misaada inayotolewa na wadau wa maendeleo na matokeo yake katika maendeleo ya  nchi.

Hayo yamesema jijini Dodoma na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. John Jingu wakati akizungumza na wajumbe wa Mkutano Mkuu Wa Asasi za KIrai Tanzania katika hotuba aliyoitoa kwa niaba ya Waziri Mkuu Mhe. Kasimu Majaliwa wakati wa ufunguzi wa Wiki ya Asasi za Kirai Tanzania.  

Dkt. Jingu aliongeza kuwa ukosefu wa uwazi na uwajibikaji wa baadhi ya AZAKI unatoa fursa ya rasilimali za umma ambazo hutolewa kwao kutumika vibaya na hivyo kuathiri kufikiwa kwa matokeo yanayotarajiwa.

Katibu Mkuu huyo aliendelea kusema kuwa hali hiyo imekuwa ikisababisha malalamiko na manung’uniko kutoka kwa wadau mbalimbali wakiwemo wafadhili wao na walengwa wa miradi yao.

“Ukosefu wa uwazi umekuwa chanzo cha migogoro miongoni mwa wanachama wa AZAKI husika.  Pia, kukosekana kwa uwazi na uwajibikaji kumesababisha baadhi ya AZAKI kutumika vibaya kinyume na sheria za nchi na kinyume malengo ya kuanzishwa kwao’’. Aliongeza Dkt Jingu.

Pamoja na mapungufu hayo Dkt. Jingu amezisifu Asasi hizo za Kiraia kuwa zinatoa mchango mkubwa katika kupambana na rushwa na ubadhirifu wa mali za umma na kuleta uwazi na uwajibikaji katika usimamizi wa mali za umma.
  Katibu Mkuu Wizara ya Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ,Dkt John Jingu akikata utepe kufungua maonesho ya Wiki ya Asasi za Kiraia Tanzania AZAKI yanayofanyika  jijini Dodoma kwa siku tano kuanzia Oktoba 22-26, 2018.
 Katibu Mkuu Wizara ya Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ,Dkt John Jingu akitoa hotuba yake wakati wa ufunguzi wa Wiki ya Asasi za Kiraia Tanzania AZAKI inayoendelea leo jijini Dodoma Kushoto ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera na Uratibu Profesa Faustine Kamuzora na kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Usajili na Uratibu Wa NGOs Bw. Leornard Baraka .
 Kaimu Msajili wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali wa  Wizara ya Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ,Bw. Leornad Baraka akijibu hoja za wadau Wiki ya Asasi za Kiraia Tanzania AZAKI yanayofanyika  jijini Dodoma kwa siku tano kuanzia Oktoba 22-26, 2018 kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ,Dkt John Jingu.
 Baadhi ya wadau wa Mkutano wa Asasi za kiraia wakifuatilia kwa makini yanayojili katika Mkutano Mkuu wa Asasi za Kiraia Tanzania AZAKI unaofanyika  jijini Dodoma kwa siku tano kuanzia Oktoba 22-26, 2018. Picha na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...