Na Vero Ignatus Arusha.
Zaidi ya wataalamu 20 kutoka katika kampuni mbalimbali za uchimbaji madini nchini wanatarajiwa kuwa mabalozi chanya katika kutoa elimu kuhusu tahadhari na matumizi sahihi ya mionzi kwa wachimbaji pamoja na jamii.
Akizungumza na wataalamu hao mkurugenzi wa tume ya nguvu za mionzi (Atomic) Profesa Lazaro Busagala nchini amesema niwakati muafaka kwa jamii kuwa na elimu,uelewa kuhusu mionzi hususani katika maeneo ya migodi na jamii inayo pakana na migodi ya uchimbaji madini.
Denis Mwalongo ni muwezeshaji wa mafunzo maalumu kwa wataalamu hao amesema kuwa katika migodi mingi nchini wafanyakazi wamekuwa wakiathirika zaidi kwa kufanya kazi zao bila vifaa vya kujikinga kiafya.
Amesisitiza kuwa endapo mionzi ikiingia Zaidi mwilini kwa muda mrefu mtu anaweza kupoteza maisha kwa kuugua hivyo ni muhimu kuchukua tahadhari kabla ya madhara kutokea katika maeneo ya kazi na jamii inayozunguka migodi ya uchimbaji madini.
Kwa upande wao baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wamesema matarajio yao baada ya kupata elimu zaidi juu ya matumizi na tahadhari kwa wafanyakazi na jamii kwa ujumla,ambapo wamesisitiza kuwa watakuwa mabalozi katika kutoa elimu hiyo ilikuokoa maisha ya wananchi na wafanyakazi wengine.
Mafunzo hayo yenye lengo la kuwajengea uwezo zaidi wataalamu hao pamoja nakuinusuru jamiii nayo inayopakana na maeneo ya migodi ilikuokoa vizazi vya sasa na vijavyo.
Zaidi ya wataalamu 20 kutoka katika kampuni mbalimbali za uchimbaji madini nchini wanatarajiwa kuwa mabalozi chanya katika kutoa elimu kuhusu tahadhari na matumizi sahihi ya mionzi kwa wachimbaji pamoja na jamii.
Akizungumza na wataalamu hao mkurugenzi wa tume ya nguvu za mionzi (Atomic) Profesa Lazaro Busagala nchini amesema niwakati muafaka kwa jamii kuwa na elimu,uelewa kuhusu mionzi hususani katika maeneo ya migodi na jamii inayo pakana na migodi ya uchimbaji madini.
Denis Mwalongo ni muwezeshaji wa mafunzo maalumu kwa wataalamu hao amesema kuwa katika migodi mingi nchini wafanyakazi wamekuwa wakiathirika zaidi kwa kufanya kazi zao bila vifaa vya kujikinga kiafya.
Amesisitiza kuwa endapo mionzi ikiingia Zaidi mwilini kwa muda mrefu mtu anaweza kupoteza maisha kwa kuugua hivyo ni muhimu kuchukua tahadhari kabla ya madhara kutokea katika maeneo ya kazi na jamii inayozunguka migodi ya uchimbaji madini.
Kwa upande wao baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wamesema matarajio yao baada ya kupata elimu zaidi juu ya matumizi na tahadhari kwa wafanyakazi na jamii kwa ujumla,ambapo wamesisitiza kuwa watakuwa mabalozi katika kutoa elimu hiyo ilikuokoa maisha ya wananchi na wafanyakazi wengine.
Mafunzo hayo yenye lengo la kuwajengea uwezo zaidi wataalamu hao pamoja nakuinusuru jamiii nayo inayopakana na maeneo ya migodi ilikuokoa vizazi vya sasa na vijavyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...