Na Ramadhani Ali – Maelezo Zanzibar 

Msaada wa Dawa na Vifaa Tiba unaotolewa na wafadhili mbali mbali unaweza kupunguza matumizi ya Serikali yaliyopangwa katika bajeti ya mwaka 2018/19 iwapo Wafanyakazi wa Wizara ya Afya watachukua juhudi ya kuilinda na kuitunza misaada hiyo. 

Waziri wa Afya Hamad Rashid Mohamed alieleza hayo Ofisini kwake Mnazimmoja wakati wa hafla ya kupokea msaada wa vifaa tiba na vitendea kazi vya Hospitali kutoka Shirika linalotoa misaada ya Kijamii la Marekani la HHRD kupitia Jumuiya ya Muzdalifa ya Zanzibar. 

Alisema Serikali inaendeleza mashirikiano na Mashirika na Taasisi za ndani na nje ya nchi ili kuona huduma za Afya zinaimarika na wananchi wanapata huduma bila usumbufu. Waziri Hamad alilipongeza Shirika la HHRD kwa msaada huo na kulishauri kuangalia uwezekano wa kusaidia zaidi katika maeneo ya mama na mtoto na kuwapatia mafunzo wafanyakazi wa Hospitali. 

Alikumbusha kuwa pamoja na misaada inayotolewa na wafadhili, Serikali imeweka Bajeti ya kutosha kwa ajili ya dawa na amewataka wafanyakazi wanaosimamia uagiziaji wa dawa kuwa waangalifu kuepuka kununua dawa ambazo zipo kwa wingi katika Hospitali na vituo vya afya. 
Katibu Mkuu Shirika la HHRD la Marekani Ayoub Mohd akimkabidhi hati ya mkabidhiano ya vifaa vilivyotolewa na Shirika hilo katika hafla iliyofanyika Wizara ya Afya Mnazimmoja, Mjini Zanzibar. 
Meneja Mkaazi wa Shirika la HHRD Ofisi ya Nairobi Musa Ibrahim akieleza kuridhishwa na watendaji wanpopkea misaada wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa vya Hospitali iliyofanyika Wizara ya Afya Mnazimmoja. 
Katibu Mkuu Shirika la HHRD Ayoub Mohd akizungumza baada ya kumkabidhi Waziri wa Afya msaada wa vifaa vilivyotolewa na Shirika hilo katika hafla iliyofanyika Wizara ya Afya Mnazimmoja Mjini Zanzibar. 
Waziri wa Afya Hamad Rashid Mohamed akitoa shukrani zake kwa Shirika la HHRD kwa msaada waliotoa kwa ajili ya wananchi wa Zanzibar. 
Waziri wa Afya Hamad Rashid Mohamed akimkabidhi mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Watu Wenye Ulemavu Zanzibar Haidar Hassan Madoea moja ya baskeli zilizotolewa msaada na Shirika la HHRD .Picha na Ramadhani Ali – Maelezo Zanzibar 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...