NA BALTAZAR MASHAKA, TARIME

ZAWADI zimetajwa kuwa chanzo na kichocheo kikubwa cha vitendo vya ukeketaji na tohara kwa watoto wa kike na kiume wilayani Tarime katika Mkoa wa Mara.

Hayo yamebainishwa na baadhi ya wanafunzi walioshiriki tamasha la kupinga Ukatili wa kijinsia lililoandaliwa na Shirika la ATFGM Masanga na kufanyika katika Shule ya Sekondari Kemambo kwa ufadhili wa Terre des Homes tamasha ambalo lilishirikisha shule 10 mbili za msingi na nane za msingi wilayani Tarime.

Wanafunzi hao walieleza kuwa kipindi cha ukeketaji mabinti (watoto wa kike) wanapotoka kukeketwa huzunguka kwenye jamii inayowazunguka ili kupatiwa zawadi ya fedha, nguo na vitu vingine jambo ambalo huwashawishi wengine ambao hawajakeketwa kwenda kufanyiwa vitendo hivyo vya ukatili ili nao wapatiwe zawadi.

Pia waliishauri serikali kusimamia Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009 na kanuni zake kupiga marufuku vishawishi vya zawadi za nguo na fedha ili kudhibiti uketetaji wa watoto wa kike na tohara isiyo salama kwa vijana wa kiume.

“Mtoto mmoja anaweza kupata nguo (vitenge) na fedha nyingi ambazo huzibana kwa pini kichwani hivyo wale ambao ni wadogo kama hawajakeketwa wakiona hizo zawadi wanatamani na kushawishika kukeketwa, hivyo serikali ipige vita zawadi hizo kwa kusimamia Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009 na kanuni ” alisema ( Maria Marwa jina la linahifadhiwa) mwanafunzi huyo wa Shule Msingi Nyabusara.
 Mwanasheria wa Shirika la Kupinga Ukatili wa Kijinsia la ATFGM Masanga wilayani Tarime, Dora Luhimbo akitoa elimu ya kupinga masuala ya ukeketaji na ndoa za utotoni lililoandaliwa na shirika hilo na kukutanisha shule 10 za msingi na sekondari ambalo lilifanyika katika Shule ya Sekondari Kemambo wilayani humo.
 Wanafunzi wa shule za msingi na sekondari za kata za Matongo na Kemambo wakiwa katika tamasha la elimu ya kupinga Ukatili wa Kijinsia, Ukeketaji, Ndoa na Mimba za utotoni lililoandaliwa na shirika la ATFGM Masanga Tarime.
 Mwanasheria wa Shirika la Kupinga Ukatili wa Kijinsia wilayani Tarime, Mara ( ATFGM Masanga) Dora Luhimbo akicheza muziki na baadhi ya wanafunzi katika tamasha hilo la kupinga ukatili wilayani humu.
Mgeni rasmi, Mkuu wa Shule ya Sekondari Kemambo Matinde Gimonge akifungua tamasha la kupinga Ukatili wa Kijinsia na kuwataka wanafunzi kuwa mabalozi wazuri wa kufikisha elimu kwa jamii, elimu ambayo wanaipata kupitia kwenye matamasha ya namna hiyo.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...