Na. Vero Ignatus, Arusha

Mgogoro uliodumu kwa takribani miaka 13 wa kanisa la AMEKI wilayani Arumeru kata ya Usariva umemalizika kwa pande mbili kukubaliana kwa kuondoa tofauti zao na kuamua kuwa na kanisa moja na uongozi mmoja

Akizungumzia mgogoro huo uliodumu kwa miaka 13 mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro amewapongeza viongozi kwa hatua kubwa waliyoifikia kwani kwa miaka yote hali ilikuwa nzito na mgogoro ulidumaza maendeleo ya kanisa ,ustawi wa wananchi,maendeleo ya shughuli za serikali katika wilaya hiyo.

"Mhe. Baba Askofu, Mhe. Msaidizi wa , Askofu nimesimama hapa kwa niaba ya serikali kuwapongeza kwa hatua kubwa mliyofikia, tumekuwa na changamoto za mgogoro uliodumu kwa miaka 13''alisema Jerry.Jerry amesema kuwa serikali itaendelea kusimama na kanisa la AMEKI kuwaunga mkono katika juhudi za kuwaletea wananchi maendeleo sambamba na ukuaji wa kiroho na maendeleo ya waumini wao

'' Ndani ya miezi mitatu kama mkuu wa wilaya namshukuru sana Mungu kunifanya kuwa chachu ya kuwapatanisha viongozi hawa wa kanisa na leo wamekuwa wamoja na kanisa moja naamini sasa baraka zaungu zitaonekana''alisema Jerry .Sambamba na hayo amesema kwakuwa mgogoro umeisha,serikali inaanza kazi mara moja ndani ya wiki moja serikali itahakikisha kuwa inatatua changamoto zote ya maeneo yote ambayo yalikuwa ya kanisa

Baadhi ya Wachungaji na viongozi wa Makanisa ya Ameki nchini waliohudhuria ibada hiyo ya shukrani wakiwa na Baba askofu pamoja na makamu wa askofu katika ibada ya pamoja
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Jerry Muro akizungumza katika la AMEKI mara baada ya pande mbili hizo kuondoa tofauti zao na kuamua kuwa wamoja na uongozi mmoja
Mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro akimpongeza Baba Askofu wa kanisa la Ameki lililopo Wilayani hapo kata ya Usariva mara baada ya kuondoa tofauri zao na kutangaza Amani


Baadhi ya waumini katika kanisa la Ameki waliohuduria katika Ibada ya shukrani baada ya mgogoto huo uliodumu zaidi ya miaka 13 kumalizika

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...