KAMPUNI ya IPP Automobile Ltd imeingia ubia na Kampuni ya Youngsan ya Korea kusini kuwekeza katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi kwa kuwa na kiwanda cha kuunganisha magari nchini.
Gari la mwanzo kutoka katika uwekezaji huo wa zaidi bilioni 22, litaingia sokoni kati ya Septemba na Oktoba mwaka 2019.
Kiwanda hicho kinachotarajiwa kuunganisha magari 1000 kwa mwaka kitatoa ajira za moja kwa moja kwa wananchi 500, idadi inayotarajiwa kuongezeka kadri ya muda unavyokwenda.
Kiwanda hicho kitajengwa eneo la Kurasini, ujenzi utaanza mwanzoni mwa mwaka ujao.
Makubaliano ya uanzishwaji wa kiwanda hicho yalitiwa saini jijini Dar es Salaam jana kati ya Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi na Bw Thomas Choi Mkurugenzi na Mwakilishi wa Kampuni ya Youngsan Glonet ya Korea ambao ndio wawakilishi wa kiufundi wa kampuni ya Zyle Daewoo Commercial Vehicle na Hyundai Motor Corporation ya Korea Kusini huku tukio hilo likishuhudiwa na Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini, Song Geum-young .
Katika mazungumzo wawakilishi hao na balozi walisema kuanzishwa kwa kiwanda hicho, kumelenga kuunga mkono juhudi za maendeleo nchini.
Akizungumzia hatua hiyo, Mwenyekiti Mtendaji  wa IPP,Dk. Reginald Mengi alisema kuanzishwa kwa kiwanda hicho, ilikuwa moja ya ndoto zake kama hatua ya kuitikia mwito wa Serikali ya Awamu ya Tano ya Rais John Magufuli, inayosisitiza kasi ya ujenzi wa viwanda nchini.
“Hakuna kinachoshindikana ukiwa na nia, hata Rais wetu anapambana katika mambo ambayo wengi waliona yanashindikana, amenunua ndege na  kufanya mengine mengi..hii ni hatua kubwa katika kukuza maendeleo yetu,” alisema Dk. Mengi.
 Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi akizungumza katika hafla fupi ya kutiliana saini hati ya makubaliano ya kuanzishwa kwa mradi kuunganisha magari hapa nchini iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi za IPP jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi na Mwakilishi wa Kampuni ya Youngsan Glonet ya Korea, Bw. Thomas Choi na kushoto Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini, Mh. Song Geum-Young.
 Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini, Mh. Song Geum-Young (kushoto) akizungumzia furaha yake kushuhudia utiaji saini huo unaounga mkono jitihada za kuigeuza Tanzania kuwa ya viwanda katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi za IPP jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi na kulia ni Mkurugenzi na Mwakilishi wa Kampuni ya Youngsan Glonet ya Korea, Bw. Thomas Choi.
 Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi (kushoto) na Mkurugenzi na Mwakilishi wa Kampuni ya Youngsan Glonet ya Korea, Bw. Thomas Choi wakitiliana saini hati ya makubaliano ya kuanzishwa kwa mradi kuunganisha magari hapa nchini katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi za IPP jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo kutoka kushoto waliosimama kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa  IPP Touchmate, Bw. Victor Tesha, Msaidizi wa Dk. Mengi, Bw. Godfrey Bitesigirwe pamoja na Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini, Mh. Song Geum-Young.
 Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi (kushoto) na Mkurugenzi na Mwakilishi wa Kampuni ya Youngsan Glonet ya Korea, Bw. Thomas Choi wakipeana mikono mara baada ya kutiliana saini hati ya makubaliano ya kuanzishwa kwa mradi kuunganisha magari hapa nchini katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi za IPP jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa  IPP Touchmate, Bw. Victor Tesha, Msaidizi wa Dk. Mengi, Bw. Godfrey Bitesigirwe pamoja na Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini, Mh. Song Geum-Young.
Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi (katikati), Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini, Mh. Song Geum-Young (wa pili kulia), Msaidizi wa Dk. Mengi, Bw. Godfrey Bitesigirwe (kulia), Mkurugenzi Mtendaji wa  IPP Touchmate, Bw. Victor Tesha (kushoto) pamoja na Mkurugenzi na Mwakilishi wa Kampuni ya Youngsan Glonet ya Korea, Bw. Thomas Choi (wa pili kushoto) wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya ya tukio la utilianaji saini hati ya makubaliano ya kuanzishwa kwa mradi kuunganisha magari hapa nchini katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi za IPP jijini Dar es Salaam.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...