Ni kupitia zoezi la ‘Treasure Hunt’
Luninga hiyo inauzwa shilingi 570,000 mtandaoni lakini mteja auziwa kwa shilingi 5,700!
Ijumaa hii bodaboda yenye thamani ya shilingi 1,850,000/- itauzwa kwa shilingi 18,500 tu kwa mteja atakayeipata. 

 Jumia imetangaza kutoa pikipiki aina ya Skymark yenye thamani ya shilingi 1,850,000 kupitia zoezi la ‘Treasure Hunt’ siku ya Ijumaa ya kesho. Zoezi hilo litafanyika kupitia App ya Jumia kwenye simu za mkononi pekee ili kutoa fursa kwa kila mtu kushiriki muda na mahali popote walipo. Mshindi mwenye bahati atakayefanikiwa kuipata pikipiki hiyo atauziwa kwa bei ya punguzo la asilimia 99 ambayo ni sawa ni shilingi 18,500 tu!

Jumia inaendesha kampeni yake kubwa kabisa ya mauzo ya mwaka inayokwenda kwa jina la Black Friday. Kampeni hii ilizinduliwa Novemba 16 na itafikia ukomo mnamo Desemba 7. Tofauti na miaka mingine ambayo Jumia hufanya Black Friday kwa siku moja tu ya Ijumaa ya Novemba 23, mwaka huu wateja watafaidi ofa za Black Friday kwa Ijumaa nne mfululizo. Lengo kubwa la kampeni hii ni kuwarahisishia wateja na watanzania kwa ujumla kufanya manunuzi yao hususani kipindi cha msimu wa sikukuu za Krisimasi na mwaka mpya ambazo zipo njiani wiki chache zijazo.

Akizungumza na waandishi wa habari, Meneja Uhusiano wa Umma wa Jumia Tanzania, Bw. Kijanga Geofrey amefafanua kuwa, “zoezi la kuficha bidhaa mtandaoni ili wateja kuzisaka na kujishindia au ‘Treasure Hunt’, ni mojawapo ya vitu vichache vinavyoendelea katika kampeni hii ya Black Friday. Miongoni mwa ofa zinazopatikana ni pamoja na punguzo la bei mpaka asilimia 70 na mauzo ya bidhaa maalum kwa bei nafuu zaidi ndani ya muda mfupi ndani ya siku au ‘Flash Sales.”
Meneja Uhusiano wa Umma wa Jumia Tanzania, Bw. Kijanga Geofrey akizungumza na Wanahabari leo jijini Dar kuhusu ufafanusi  wa  “zoezi la kuficha bidhaa mtandaoni ili wateja kuzisaka na kujishindia au ‘Treasure Hunt’,alisema na kuongeza kuwa ni mojawapo ya vitu vichache vinavyoendelea katika kampeni hii ya Black Friday. Kijanga amebainisha kuwa Miongoni mwa ofa zinazopatikana ni pamoja na punguzo la bei mpaka asilimia 70 na mauzo ya bidhaa maalum kwa bei nafuu zaidi ndani ya muda mfupi ndani ya siku au ‘Flash Sales.”



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...