Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kama mnavyofahamu linashiriki Ulinzi wa Amani ndani na nje ya Bara la Afrika.
JWTZ linasikitika kuwataarifu kwamba limewapoteza wapiganaji wake watatu (3) waliofariki kwa tarehe tofauti nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Afrika ya Kati (CAR) wakiwa kwenye jukumu la Ulinzi wa Amani baada ya kushambuliwa na vikundi vinavyosadikiwa kuwa ni vya waasi.
Mashujaa wetu waliouwawa ni Koplo Mohamed Mussa, Koplo Erick Masauri John na Praiveti Musa Shija Machibya. Miili ya marehemu hao tayari imepokelewa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere na kuhifadhiwa katika Hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo.
Heshima za mwisho kwa mashujaa wetu hao zitatolewa katika sehemu ya kuagia Hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo kesho tarehe 23 Novemba 2018 kuanzia saa 2.30 asubuhi. Vyombo vya Habari na Wananchi wanakaribishwa tuungane katika kuaga mashujaa wetu.
Mungu azilaze Roho za Mashujaa wetu mahali pema Peponi, Amina.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...