CHAMA cha Riadhaa nchini (RT), kimetoa baraka kwa wandaaji was mbio za kujifurahisha Mbezi Fun Run zilizopangwa kufanyika Desemba Mosi jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu wa RT, Willihelmi Gudagudai alisema RT imetoa kibali kwa wandaaji hao baada ya kufuata taratibu zote."Tumewataka baada ya tamasha lao, wawasiliane na RT ili mbio zao ziingizwe kwenye kalenda ya mwaka ya matukio ya RT."alisema.

Kwa upande wa waandaji hao kupitia kwa katibu Mbezi Fun Run Omary Kimbau alisema mandalizi ya mbio hizo yamekamilika kwa asilimia 90 mpaka Sasa, na kwamba kuanzia leo wataweka wazi vituo mbali mbali vya kujiandikisha kwa yeyote anayependa kushiriki.

"Kushiriki ni bure, hakuna kingilio chochote na mlango upo wazi kwa yeyote, ila kuna tisheti na beji kwa wakimbiaji, beji shilingi 10,000 na atakayependa kutumia fulani zetu bei ni shilingi 25,000."alisema.Kimbau alisema mbio hizo zimeandaliwa na umoja wa wakazi wa Mbezi Beach zikiwa na lengo la kufahamiana na kubadilishana mawazo na kusaidia kwenye changamoto mbali mbali huku mgeni rasmi akitarajiwa kuwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Ummy Mwalimu.

“Kama mnavyojua siku hiyo ya Desemba Mosi itakuwa ni siku ya ukimwi duniani hivyo pia tumemualika Waziri Ummy Mwalimu awe mgeni rasmi na tutafanya nae mazoezi ya pamoja, na pia kutakuwa na zoezi la uchangiaji damu.“Damu salama inahitajika kwenye banki ya damu, kama haijanisaidia mimi itamsaidia ndugu yangu, jamaa au mtanzania yoyote yule, hivyo tumeona siku hiyo pia tuitumie kuchangia damu salama na pia kupima afya yetu kwa kupima maambukizi ya virusi ya ukimwi.”alisema.


Pichani kati ni mwenyekiti wa bonaza hilo la Mbezi Run Fun Loraa George ‘Robelo’ alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya mbio hizo ambazo anaeleza kuwa kwa asilimia 90 yamekamilika,kulia ni Katibu wa Mbezi Fun Run Omary Kimbau na kushoto ni mwakilishi kutoka kitengo cha afya Wilaya ya kinondoni Getruda Kafuko.
Katibu wa Mbezi Fun Run Omary Kimbau akizungumza mbele ya Waandishi wa Habari jana kuhusu kukamilika kwa maandalizi ya mbio hizo  kwa asilimia 90 mpaka Sasa,na kuongeza kuwa vitakuwepo vituo mbali mbali vya kujiandikisha kwa yeyote anayependa kushiriki.

"Kushiriki ni bure, hakuna kingilio chochote na mlango upo wazi kwa yeyote, ila kuna tisheti na beji kwa wakimbiaji, beji shilingi 10,000 na atakayependa kutumia fulani zetu bei ni shilingi 25,000."alisema.Kimbau alisema mbio hizo zimeandaliwa na umoja wa wakazi wa Mbezi Beach zikiwa na lengo la kufahamiana na kubadilishana mawazo na kusaidia kwenye changamoto mbali mbali huku mgeni rasmi akitarajiwa kuwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Ummy Mwalimu.
Mkurugenzi wa ufundi wa mbio za Mbezi Fun Run Isihaka Mlawa akionesha kibali walichopewa mara baada ya kufuata na kukamilisha taratibu zote kutoka chama cha Riadhaa nchini (RT).

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...