WAZIRI MKUU Kassim Majaliwaamewaagiza Warajisi Wasaidizi wa Ushirika katika Mikoa yote inayolima korosho nchini waandae semina kwa Maafisa Ushirika, viongozi wa vyama vya msingi (AMCOS), maafisa ugani na wakulima ili kuwawezesha kubaini na kupanga korosho katika madaraja kuanzia ngazi ya vyama vya msingi.
Amesema jambo hilo litasaidia mkulima aweze kujua korosho aliyoipeleka ina ubora gani akiwa huko kijijini na wanapoifikisha kwenye ghala kuu wafanye kazi ya kuthibitisha , kwa hatua hiyo itasaidia kuondoa malalamiko kuhusu madaraja .
“Zoezi hili licha ya kuthibitisha ubora itasaidia kuboresha uzalishaji kwani wakulima wataelimishwa namna ya kuimarisha na kuboresha uzalishaji wa korosho nchini ikiwa ni pamoja na matumizi bora ya viatilifu ’’
Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumatano, Novemba 21, 2018) wakati alipotembelea kiwanda cha korosho cha BUKO kilichopo kwenye Manispaa ya Lindi, ambapo ameshuhudia korosho zikipimwa ubora kwenye ghala kuu lilipo kiwandani hapo.
Ameagiza semina ifanyike mwakani ili maafisa ushirika baada ya kupata mafunzo wawasaidie wakulima kwenye msimu ujao watambue korosho walizopeleka kuziuza zina ubora gani.
Waziri Mkuu amesema katika semina hiyo wakutane maafisa kilimo na maafisa ushirika ili wapate taaluma hiyo itakayowawezesha kupima korosho na kuitenga katika madaraja na kuwaondolea shida wakati wa mauzo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua uwanja wa michezo wa Ilulu uliopo
mjini Lindi, Novemba 21, 2018. Kushoto kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi,
Godfrey Zambi. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua uwanja wa michezo
wa Ilulu uliopo mjini Lindi, Novemba 21, 2018. Kushoto kwake ni Mkuu
wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua kiwanda cha korosho BUKO cha mjini
Lindi ambacho kimesimamisha uzalishaji, Novemba 21, 2018. Kushoto ni
Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua magunia ya korosho yaliyohifadhiwa
kwenye ghala la kiwanda cha korosho cha BUKO cha mjini Lindi wakati
alipotembelea kiwanda hicho, Novemba 21, 2018. Kushoto ni Mkurugenzi
wa Kampuni ya Namgongo Holding iliyopewa dhamana ya kutunza ghala hilo,
Ramadhani Katau.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akishuhudia wakati , Afisa anayesimamia Ubora
wa Korosho, Dastan Milazi alipokuwa akipima korosho zilizopokelewa
kwenye ghala la kiwanda cha korosho cha BUKO cha mjini Lindi wakati
alipotembelea kiwanda hicho kilichosimamisha uzalishaji, Novemba 21,
2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...