Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma

Aliyewahi kuwa Waziri wa Kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba ambaye ni Mbunge wa Buchosa Mkoani Mwanza leo tarehe 22 Novemba 2018 amemkabidhi rasmi ofisi Waziri wa kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb).

Makabidhiano hayo yamefanyika katika Ukumbi wa mikutano maarufu kama Kilimo IV Jijini Dodoma na kuhudhuriwa na Naibu mawaziri wa Kilimo Mhe Omary Mgumba na Mhe Innocent Bashungwa, Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe, na Wakuu wa idara na Vitengo.

Akizungumza katika hafla hiyo fupi Mhe Dkt Tizeba amempongeza Mhe Hasunga kwa kuteuliwa kuhudumu katika nafasi hiyo ambapo amesisitiza kusimamiwa kwa weledi huduma za ugani ambazo kwa kiasi kikubwa hakuna jambo la kujivunia katika eneo hilo kutokana na mgawanyo wa kimajukumu kuwa katika wizara mbili ya kilimo na TAMISEM jambo ambalo linapunguza ufanisi wa kiweledi.

Alisema kuwa wizara inapaswa kuendelea kusomesha wataalamu mbalimbali nchini wakiwemo wa ugunduzi na utafiti ili kuongeza tija ya kilimo na utoaji elimu kwa wakulima na kuongeza uwezo wa uzalishaji wa wananchi sambamba na Taifa kwa ujumla.
Mbunge wa Buchosa Mkoani Mwanza Mhe Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Kulia) akifurahi jambo pamoja na Waziri wa kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) wakati wa hafla ya makabidhiano ya Ofisi Jijini Dodoma leo tarehe 22 Novemba 2018. (Picha Zote Na Mathias Canal-Wizara ya Kilimo).
Waziri wa kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akizungumza na wafanyakazi wa Wizara ya kilimo wakati wa hafla ya makabidhiano ya Ofisi Jijini Dodoma leo tarehe 22 Novemba 2018. 
Picha ya pamoja waziri wa kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb), Mbunge wa Buchosa Mkoani Mwanza Mhe Mhandisi Dkt Charles Tizeba, Naibu mawaziri wizara ya kilimo Mhe Omary Mgumba na Mhe Innocent Bashungwa, na Katibu Mkuu wa Wizara ya kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wote wakati wa hafla ya makabidhiano ya Ofisi Jijini Dodoma leo tarehe 22 Novemba 2018. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...