Na Pamela Mollel,Arusha
Banc ABC katika kuwajali wateja wake wa maeneo mbalimbali hapa nchini imeanzisha huduma maalumu ya kutumia satellite ili kuwafikia kwa haraka zaidi
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha hivi karibuni, Meneja wa Benki hiyo Magabe Nyambuche alisema pamoja na kuboresha huduma za kibenki pia wameanzisha huduma hiyo ya satelite itakayokuwa na uwezo wa kuwafikia hata wateja wavijijini
Alitaja mikoa ambao kwa sasa wanatoa huduma hiyo ya satellite ni Arusha,Dar es salaam,Dodoma na Mwanza.Alisema kuwa katika msimu huu wa sikukuu ya Chrismas wanatoa zawadi kwa wateja wote watakao weka pesa kwenye account(fixed account)watapata riba papo kwa papo.Pia aliwataka wananchi kujiunga na benki hiyo kwakuwa huduma zake ni nzuri .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...