Benki ya Azania imezidi kujitanua baada ya hii leo kuzindua tawi lake jipya jijini Dodoma ikiwa ni muendelezo wa mkakati wa benki hiyo katika kukuza mtatandao wa matawi yake sambamba na kuunga mkono jitihada za Mh Rais John Magufuli kuifanya Tanzania kuwa nchi ya Viwanda, kupitia huduma bora za kibenki.

Akizungumza kwenye hafla fupi ya Uzinduzi wa tawi hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Charles Itembe alisema kwa sasa benki hiyo ina matawi kumi na tisa ikiwemo tawi hilo jipya lililopewa jina la Sokoine- Dodoma ikiwa ni ishara ya benki hiyo kutambua mchango wa Waziri Mkuu wa zamani, Hayati Edward Moringe Sokoine katika ustawi wa taifa kwa ujumla.

“Malengo yetu ya kimkakati kwa sasa ni kukuza mtatandao wa matawi ya benki yetu , angalau matawi matatu kwa mwaka, na pia kukuza nafasi yetu ya umiliki wa soko( Market share) angalau kwa 3% ndani ya miaka mitatu.’’ Alisema Bw Itembe. Alisema nia ya benki hiyo ni kuwa katika hadhi ya Mabenki Makubwa daraja la kwanza( Tier One ) ndani ya miaka hii mitano ya kimkakati wa kibiashara.

Akizungumzia uamuzi wa kufungua tawi hilo jijini humo, Bw Itembe alisema: “Dodoma ni katikati ya nchi, pili ni makao makuu ya shughuli za kiserikali na pia ni mkoa unaokuwa kwa kasi kibiashara.’’ Aidha, alibainisha kuwa kupandishwa hadhi kwa manispaa ya Dodoma na kuwa jiji kumeiweka benki hiyo katika nafasi nzuri kwa kuwa ukuaji wa jiji hilo unaendana sambamba na mahitaji ya kifedha.

“Katika kuunga mkono sera ya Mh Rais John Magufuli ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya Viwanda, ni lazima kuwa na mbinu ya kuweza kukuza kipato kupitia kufanya biashara na benki zenye msingi imara… Azania Benki tupo tayari kushirikiana na wananchi na serikali katika kufanikisha hilo,’’ alisema.

Akizungumza muda mfupi kabla hajazindua rasmi tawi hilo, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Ashatu Kijaji mbali na kuipongeza menejimenti ya benki hiyo, alitoa changamoto kwa taasisi za fedha hapa nchini ikiwemo benki hiyo kuhakikisha zinajipanga kikamilifu kukabiliana na suala la mikopo chechefu sambamba na kupunguza gharama za uendeshaji ili ziweze kuwahudumia wateja wake kwa gharama za chini zaidi ikilinganishwa na hali ilivyo sasa.
 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Ashatu Kijaji (katikati) akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa tawi jipya la benki ya Azania linalofahamika kwa jina Sokoine-Dodoma wakati wa hafla fupi ya uzinduzi huoiliyofanyika jijini Dodoma leo. Wanaoshuhudia ni pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Charles Itembe (kushoto) na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa benki hiyo, Bw Eliud Sanga. 
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa benki ya Azania Bw Eliud Sanga (wa pili kushoto) akikabidhi zawadi maalum aliyoandaliwa iliyoandaliwa kwa ajili ya Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Ashatu Kijaji (wa pili kulia) wakati wa hafla hiyo. Wanaoshuhudia ni pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Charles Itembe (kulia). 
 Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya Azania ,  Charles Itembe akizungumza kwenye hafla hiyo. 
 Baadhi ya wafanyakazi wa benki ya Azania wakifuatilia matukio mbalimbali ikiwemo hotuba ya Naibu Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Ashatu Kijaji wakati wa hafla hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...