Chama cha Waajiri Tanzania (ATE),
Disemba 14 2018 kimeandaa Tuzo za Mwajiri Bora wa Mwaka 2018
zilizofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mlimani City. Tangu
kuanzishwa kwake mwaka 2005, tuzo hizo zimejikita katika kutambua
waajiri wenye misingi bora ya usimamizi wa guvu kazi na rasilimali watu
kwa lengo la kuwawezesha kutimiza wajibu wao kikamilifu na kupelekea
kukuza uzalishaji wa kibiashara.
Tuzo hizo zilihudhuriwa na wadau
mbali mbali wakiwemo Mh. Jenista Mhagama, Mh. Anthony Mavunde, Mhe.
Stella Ikupa, Mkuu wa Mkoa DSM, Mhe. Paul Makonda, Balozi wa Norway
nchini, Bi. Elisabeth Jacobsen, Balozi wa Denmark nchini, Bw. Einer H.
Jensen na Balozi wa China nchini Nd. Wang Fe, pamoja na taasisi mbali
mbali ikiwemo TUKTA na ILO.
Tuzo hizo zinazofanyika kila
mwaka zimasaidia kuhamasisha wanachama kuchukulia masuala ya ajira na
usimamizi wa rasilimali watu kama misingi muhimu katika kumwezesha
mwajiri kuwana wafanyakazi wenye uwezo na ueledi ili kukidhi mahitaji ya
ushindani katika biashara.
Sherehe ya utoaji tuzo
iliyohudhuriwa na Mhe. Jenista Mhagama (MB) Waziri wa Nchi Ofisi ya
Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu akiwa
Mgeni Rasmi, zimekuwa maarufu hapa nchini katika muktadha wa biashara
hasa kwa kuhamamasisha makampuni makubwa na madogo na ya ukubwa wa kati
kuhusu umuhimu wa kuzingatia misingi bora ya kufanya biashara nchini.
Mwenyekiti wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Bi. Jayne Nyimbo-Taylor akihutubia wageni waalikwa katika hafla ya kutoa Tuzo ya Mwajiri Bora wa Mwaka 2018 iliyoandaliwa na chama hicho katika ukumbi wa Mlimani City, tarehe 14 Disemba. Hafla hiyo iliyohudhuriwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama (MB) akiwa mgeni rasmi ilitoa tuzo kwa kutambua vipengele 17 kutambua waajiri wenye misingi bora ya usimamizi wa nguvu kazi na rasilimali watu.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama (MB) akihutubia wageni waalikwa katika hafla ya Tuzo ya Mwajiri Bora wa Mwaka 2018 iliyoandaliwa na Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE) katika ukumbi wa Mlimani City. tarehe 14 Disemba. Hafla hiyo iliyohudhuriwa na wadau mbali mbali wakiwemo Mh. Anthony Mavunde (MB), Mhe. Stella Ikupa (MP), wawakilishi wa balozi za Norway, Denmark, China pamoja na taasisi mbali mbali ikiwemo TUKTA na ILO na waajiri mbali mbali nchini.
Mwakilishi wa Tanzania Cigarette Company (TCC), akipokea Tuzo ya Mwajiri Bora wa Mwaka 2018 baada ya kampuni hiyo kuibuka washindi afasi ya tatu katika hafla iliyoandaliwa na Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE) katika ukumbi wa Mlimani City, tarehe 14 Disemba mgeni rasmi akiwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama (MB).
Mwakilishi wa Tanzania Breweries Limited (TBL), Bi. Lilian Makau akipokea Tuzo ya Mwajiri Bora wa Mwaka 2018 baada ya Kampuni hiyo kuibuka washindi nafasi ya pili katika hafla iliyoandaliwa na Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE) katika ukumbi wa Mlimani City, tarehe 14 Disemba mgeni rasmi akiwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama (MB).
Wafanyakazi wa Geita Gold Mine (GGM) wakifurahiya Tuzo ya Mwajiri Bora wa Mwaka 2018 pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama (MB) baada ya kampuni hiyo kuibuka washindi nafasi ya kwanza kwenye hafla iliyoandaliwa na Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE) katika ukumbi wa Mlimani City, tarehe 14 Disemba 2018.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...