NA MWAMVUA MWINYI, KIBAHA 

MKUU wa wilaya ya Kibaha, Assumpter Mshama amesema ataandika ombi la kufuta hati ya shamba la mmiliki Siemens, lililopo kata ya Pangani, kutokana na kuwa pori na kugeuzwa jalala la kutupwa miili ya marehemu pamoja na kutumika kwa uhalifu. 

Hatua hiyo inakwenda pamoja na kuwakabidhi wananchi kulitumia kwa masharti ya kulima mazao ya muda mfupi wakati serikali ikiendelea na taratibu za kupima viwanja na kuuza kwa gharama nafuu. 

Akitoa maamuzi hayo wakati alipokuwa akizungumza na wananchi wa kata hiyo, Assumpter alisema ifikie mwisho kujaza viwanja na mashamba pori wilayani hapo. Assumpter alitoa rai kwa wamiliki wenye mashamba na viwanja pori kuanza kuyaendeleza na kama watakaidi wananchi wakiyavamia ataruhusu wagawiane maeneo. 

"Hii ni salamu tuu, mwenzio akinyolewa wewe anza kutia maji, wananchi wamechoshwa kulinda maeneo ya watu, kama mmeyashindwa yaacheni"alifafanua Assumpter. Awali diwani wa kata ya Pangani, Agustino Mdachi aliomba serikali ,kuangalia namna ya kufuta umiliki wa mashamba ambayo hayaendelezwi na kusababisha kutumika vificho vya wahalifu .

Alisema, kwa kipindi cha miezi sita miili zaidi ya kumi zimeokotwa kwenye mtaa huo ambapo kati yao wengine walinusurika kifo na kuokolewa na wengine wakiwa wamefariki dunia. Nae mwenyekiti wa mtaa wa Pangani Jitihada Ndiali alisema maeneo hayo yamegeuzwa dampo au sehemu ya kutupia maiti pia madereva bodaboda kuporwa pikipiki zao kisha kutupwa .

Kwa upande wa wananchi akiwemo Lillian Godfrey alimpongeza mkuu wa wilaya kwa maamuzi yake. Alisema, wamekubali kulima mazao ya muda kama mihogo, mbaazi, maharage na mbogamboga hadi hapo serikali itakapofanya maamuzi ya moja kwa moja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...