Mkuu wa wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Sophia Mfaume Kizigo ameiagiza taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU wilayani Namtumbo kuchunguza shilingi milioni 950 zilizobadilishiwa matumizi na Halmashuri ya Namtumbo.

Kizigo aliyasema hayo hivi karibuni katika mkutano wa baraza la madiwani wilayani humo baada ya kubaini baraza la madiwani kutoridhika na taarifa ya mkaguzi wa ndani wa Halmashauri hiyo juu ya kubadilisha matumizi ya fedha shilingi milioni 950.

Taarifa ya mkaguzi wa ndani wa Halmashuri hiyo bwana John Mwingira ilidai Halmashuri hiyo imebadilisha matumizi ya fedha kiasi cha shilingi milioni 950 na kutumika kwa matumizi mengineyo tofauti na ilivyokusudiwa .

Aidha bwana Mwingira katika taarifa yake hiyo alidai kuwa fedha hiyo imetumika kwa nia njema lakini zinatakiwa kurudishwa katika shughuli iliyokusudiwa na serikali kwa kutumia mapato ya ndani ambayo kwa sasa yanasuasua.

Taarifa hiyo ilisema katika shilingi milioni 950 milioni 500 zilikuwa Ruzuku ya serikali zikiwa na lengo la kujenga Hospitali ya wilaya ambapo katika fedha hiyo milioni 200 zilibadilishwa matumizi na kumalizia zahanati saba viporo vya Halmashuri hiyo na kuanza kutumika na milioni 20 nazo zilibaki kujenga jengo moja katika Hospitali ya wilaya na milioni 156 zilipelekwa kukamilisha chumba cha upasuaji katika kituo cha afya lusewa katika mamlaka ya mji mdogo wa Lusewa.

Milioni 450 kati ya hizo milioni 950 zilipokelewa na Halmashuri hiyo kutoka bodi ya mikopo ya serikali za mitaa LGLB ambazo nazo zililenga kujenga soko zilibadilishwa matumizi na kulipia deni la vifaa vya viwandani milioni 214 zilizokopa Halmashuri hiyo na milioni 26 zilitumika kununulia mashine ya kukusanyia ushuru (POS)ishirini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...