Na. Lorietha Laurence-WHUSM,Dodoma
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe amesema kuwa lugha ni kielelezo na  sehemu  muhimu ya utambulisho wa taifa  lolote duniani. Hayo ameyasema jana Jijini Dodoma  katika Hafla  ya  kuwatunuku vyeti vya utambuzi wataalamu 67 wa lugha ya Kiswahili waliofuzu mafunzo ya muda mfupi yaliyoandaliwa  na  Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA).
“Taifa lolote lisilo na utamaduni wake ni taifa mfu, na sisi tunajivunia kwa kuwa na utamaduni hai ikiwemo lugha yetu ya Kiswahili” alisema Dkt. Mwakyembe Aidha aliongeza kwa kueleza kuwa  lugha ya Kiswahili ni kitambulisho cha utamaduni wa Mtanzania , kwa kuwa ndiyo lugha inayowaunganisha watu katika shughuli mbalimbali za Kijamii, Kisiasa na kiuchumi. Dkt. Mwakyembe anazidi kufafanua kuwa takribani lugha elfu sita (6000) huzungumzwa kila siku  duniani  ambapo  lugha ya Kiswahili  ni miongoni mwa lugha 10 zinazoongelewa kwa wingi.
“Mafunzo haya ni mwanzo tu mwa mambo mengi mazuri ambayo Wizara yangu imepanga kufanikisha na ukizingatia kampeni ya mwaka huu ya Uzalendo na Utaifa ina kauli mbiu inayohamasisha kukuza lugha yetu ambayo ni Kiswahili Utashi Wetu, Uhai Wetu” alisema Dkt. Mwakyembe.
Naye Kaimu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) Bibi.
 Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akiongea na  wataalamu wa lugha ya Kiswahili ( Hawapo katika picha),  jana Jijini Dodoma katika halfa ya kuwatunuku vyeti vya utambuzi wataalamu 67 waliofuzu mafunzo ya muda mfupi yaliyoandaliwa  na  Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) jana Jijini Dodoma..
 Mhitimu ambaye ni Mwalimu wa shule ya Sekondari Chikole ya Jijini Dodoma Bibi. Neema Mkobalo akisoma risala  kwa mgeni rasmi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison  Mwakyembe (Wa tatu kulia) katika halfa ya kuwatunuku vyeti vya utambuzi wataalamu 67 wa lugha ya Kiswahili waliofuzu mafunzo ya muda mfupi yaliyoandaliwa  na  Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) jana Jijini Dodoma.
 Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (Kulia)  akimkabidhi cheti  mmoja wa wahitimu wa mafunzo ya muda mfupi ya  wataalamu wa lugha ya Kiswahili  Mwalimu  wa Shule ya Msingi Chikowa  Bibi. Theresia Lejale jana Jijini Dodoma.
 Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (Kulia)  akimkabidhi cheti  mmoja wa wahitimu wa mafunzo ya muda mfupi ya  wataalamu wa lugha ya Kiswahili  Mwalimu wa  wa Shule ya Msingi Vikonje  Bw. Emmanuel Mzumya jana Jijini Dodoma.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...