Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
Siku hii ya Kimataifa ya Wahamaji huadhimishwa Duniani kote tarehe 18/12 kila mwaka ikiwa ni kutambua mchango wa Wahamaji katika kukuza uchumi wa nchi za ugeni (horst country) na wanakotoka (origin) kadhalikaa kuheshimu uhuru na haki zao za kibinadamu.
Katika maadhimisho ya Mwaka huu yanapambwa na kauli mbiu isemayo Uhamaji unaozingatia Utu.
Akizungumza na Michuzi Blog Msemaji wa Idara hiyo Ally Mtanda amesema kuwa katika kuadhimisha siku hii, Idara ya Uhamiaji inafanya Maonesho maalum katika Viwanja vya Mnazi Mmoja kwa kutoa pasipoti za kielektroniki kwa Watanzania.
Aidha, elimu kwa Umma kuhusu Uraia, Viza na Vibali vya Ukaaazi itatolewa. Pia Wananchi watapata fursa ya kujua mafunzo yanayotolewa na Chuo cha Uhamiaji cha Kikanda Moshi (Tanzania Regional Immigration Training Academy-TRITA)
"Ninawasihi Watanzania, Taasisi, Makampuni na Mashirika mbalimbali kutumia fursa ya maonesho haya kupata huduma zetu kwa kufika wenyewe na kuepeukana na vishoka" Aliongeza Mtanda.
Maadhimisho hayo huanza Desemba 16 na kufikia kilele chake Desemba 17.
Picha
ya pamoja wafanyakazi wa Idara ya Uhamiaji katika maadhimisho ya Siku
ya Kimataifa ya Wahamaji Duniani yanayofanyika katika viwanja vya Mnazi
Mmoja Jijini Dar es Salaam.
Mrakibu
Msaidizi wa Idara ya Uhamiaji Grace Rutachokozibwa akitoa huduma katika
maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wahamaji Duniani yanayofanyika
katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...