Jaji mkuu wa Tanzania Mh. Ibraham H. Juma, amekitaka Chuo Cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) kufanya tafiti na kutoa ushauri wa namna ya kuondoa migongano ya kisheria wakati Mahakama ikiendelea kuangalia namna bora ya kusimamia sheria ili kupunguza au kuondoa kabisa migongano hiyo.
Mh. Jaji Mkuu ametoa agizo hilo leo wakati akizindua baraza la tatu la wafanyakazi la Chuo Cha (IJA), katika hafla ya uzinduzi wa balaza hilo, iliyofanyika katika ukumbi wa Kituo cha Kumbukumbu Tuli cha Taifa jijini Dododma.
Kupitia hotuba yake Mh. Jaji Mkuu, mbali na kuzitambua changamoto zinazokikabili Chuo hicho, ikiwemo upungufu wa vitendea kazi na watumishi kwa kada ya utawala, aliwakumbusha watumishi wa Chuo hicho kuzingatia uadilifu katika kutekeleza shughuli zao za kila siku.
“Tunawajibika kufanya kazi kwa weledi, uthubutu na uadilifu wa hali ya juu, ili tuwawakilishe vyema wale waliotuamini sambamba na kuiwezesha serikali kufikia malengo yake ya kukuza uchumi wa viwanda na kuondoa umasikini” alisistiza Mh. Jaji Mkuu.
Jaji
Mkuu wa Tanzania Prof.Ibrahim Hamis akizungumza wakati wa akizindua
Baraza la tatu la wafanyakazi la Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto
Leo Jijini Dodoma. Kulia kwake ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya
Tanzania Kanda ya Dodoma Mhe.Ignas Kitusi na Kushoto kwake ni Mkuu wa
Chuo na Mwenyekiti wa Baraza hilo Jaji Dkt Paul Kihwelo.
Baadhi
ya wajumbe wa Baraza la wafanyakazi la Chuo cha Uongozi wa Mahakama
Lushoto wakifuatilia hotuba ya Jaji Mkuu wa Tanzania Prof.Ibrahim
Hamis(hayupo pichani) wakati akizindua Baraza la tatu la wafanyakazi la
Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto Leo Jijini Dodoma.
Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Hamis akiwa kwenye picha ya pamoja
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...