ALFRED MGWENO (TEMESA TANGA) 

Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA Mhandisi Japhet Y. Maselle, amehitimisha ziara yake mkoani Tanga kwa kuwataka watendaji na viongozi wa Wakala mkoani humo kuendelea kufanya kazi kwa bidii na weledi mkubwa ili kuinua mapato ya kituo hicho.

Akizungumza na wafanyakazi wa TEMESA Tanga pamoja na mafundi wa karakana mara baada ya kuwasili mkoani humo, mhandisi Maselle aliwasisitizia suala la ubunifu hasa katika upande wa karakana ambapo aliwataka kuiga mfano kutoka mkoa wa Singida ambao uzalishaji wake umeongezeka kwa kipindi cha hivi karibuni kutokana na kubuni njia mbalimbali ili kuongeza pato lake ikiwemo kuepuka kupeleka kazi ndogo ndogo za ufundi katika karakana teule. 

Vilevile alipata pia fursa ya kusikiliza changamoto mbalimbali wanazokutana nazo katika utendaji kazi wao pamoja na kukagua baadhi ya mitambo iliyopo katika karakana hiyo. Changamoto kubwa iliyoonekana ilikuwa ni uchakavu wa mitambo ambapo Mhandisi Maselle alisema kuwa ni vyema sasa Wakala ukaanza utaratibu wa kununua mitambo mipya ili kuongeza ufanisi zaidi upande wa Ukodishaji mitambo. 
Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle kulia akitoa maagizo wakati akikagua gari ya kubeba mitambo mbalimbali (low bed truck) katika karakana ya TEMESA mkoa wa Tanga wakati wa ziara yake mkoani humo kukagua utendaji kazi na kusikiliza kero mbalimbali zinazowakabili wafanyakazi wa wakala huo. Kushoto ni Kaimu Meneja Mhandisi Mhangaiko Ngoroma. 
Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle akikagua Propela ya kivuko cha MV. PANGANI II ambacho kinafanyiwa ukarabati mkubwa katika yadi ya Songoro, kivuko hicho kinatarajiwa kuungana na kivuko cha MV. TANGA kutoa huduma katika eneo la Pangani na Bweni katika eneo la mto Pangani mara baada ya kukamilika kwa matengenezo yake. Nyuma yake ni Mkuu wa Kivuko cha Pangani Bweni Mhandisi Abdulrahman Ameir. 
vuko cha MV. TANGA kinachotoa huduma katika mto Pangani, kati ya Pangani na Bweni wilayani Pangani mkoani Tanga kikielea majini wakati kikiendelea kutoa huduma ya kuvusha abiria na magari. 
Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle wa pili kushoto akisisita umuhimu wa kuzingatia usalama wa vivuko kwa wafanyakazi wa kivuko hicho wakati wote wanapotoa huduma hiyo katika kivuko cha MV TANGA kinachotoa huduma katika mto Pangani, kati ya Pangani na Bweni wilayani Pangani mkoani Tanga wakati wa ziara yake ya kukagua usalama wa vivuko. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...