Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii


MRADI wa malezi na makuzi kwa watoto (Play lab Program) wamefanya maadhimisho ya mahafali ya pili ya watoto kwa mwaka 2018 uliotekelezwa na Shirika la Brac Tanzania na jumla ya watoto 1200 wamefanikiwa kumaliza mafunzo hayo.

Mradi huo wa malezi na makuzi kwa watoto hujifunza kupitia elimu ya malezi kwa wazazi, ulinzi na usalama kwa watoto.

Akizungumza wakati wa mahafali hayo, Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke John Bwana amesema elimu waliyoipata watoto hawa ni msingi mkubwa katika kuwaandaa na elimu ya awali na wenine shule ya Msingi ambapo imetia chachu katika kuwaimarisha watoto katika maendeleo ya kiakili , kimwili, kihisia na lugha.

John amesema, kupitia mradi huu wazazi wa watoto wamepewa mafunzo ya malezi kwa watoto wao kwani ni muhimu sana kwa sababu msingi wa ukuaji wa motto huanzishwa na mzazi mwenyewe.

Pia. Amesema wazazi wamekuwa mstari wa mbele katika kushiriki kazi mbalimbali za mradi kama utenenezaji wa vifaa vya asili kwa ajili ya watoto kutumia katika mafunzo yao na hii imesaidia katika kuwajenga watoto wetu kuwa na ujasiri , ukakamavu, kujiamini, kuchangamana na watoto wengine , kuwa na nidhamu bora na hata kuwa na msaada kwa wazazi wake.

Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke John Bwana akitoa vyeti kwa watoto waliohitimu mafunzo ya malezi na makuzi (play lab) unaoratibiwa na Shirika la Brac Nchini wakati wa mahafali ya pili yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.Mtathmini wa mradi wa malezi na makuzi (play lab) Lilian Josephat akitoa risali wakati wa maadhimisho ya mahafali ya pili ya watoto kwa mwaka 2018 uliotekelezwa na Shirika la Brac Tanzania na jumla ya watoto 1200 wamefanikiwa kumaliza mafunzo hayo.Watoto wakiwa katika matukio tofauti.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...