Na. Vero Ignarus, Arusha

Msenaji wa Serikali Dkt Abbas amesema serikaki inaendelea na ukarabati na ujenzi wa Zahanati na Vituo vya afya kwa nchi nzima kwani Mpango wa serikali ni kuhakikisha kila Wilaya ina hospitali

Amesema upatikanaji wa dawa umeongezeka kwa rikali kuongeza bajeti ya madawa kutoka bill.31 hadi bil. 280,ambapo Serikali inanunua madawa moja kwa moja kutoka viwandani na sio kwa madalali tena. Tiba za kibingwa zimeimarishwa sana katika nchi yetu hasa magonjwa ya Moyo,kupandikiza figo na matatizo yakutosikia hii imepelekea kupungua kwa idadi ya wagonjwa wakutibiwa nje ya nchi.

Kwa upande wa sejta ya Elimu Dkt Abbas anesema Serikali inatoa fedha kiasi cha bil.29 kila mwezi kuwezesha elimu bure katika nchi yetu.Dkt.Abbas.Amesisitiza kuwa Migomo ya elimu ya juu imeshaisha katika awamu hii ya tano kwani fedha zinapelekwa kwenye vyuo kwa wakati ambapo kwa mwaka huu kiasi cha bil 137 kimeshapelekwa kwenye vyuo mbalimbali nchini.

Amesema kuwa kwenye sekta ya Kilimo Serikali imeanzisha mamlaka ya udhibiti wa masoko kwa bidhaa za Tanzania, hii itawasaidia wakulima, wafanyabiashara kupata masoko yenye uhakika.June mwaka huu Serikali lizindua mpango mpya wa kilimo cha kisasa cha umwagiliaji ili kumuwezesha mkulima kutotegemea mvua.


Dr. Hassan Abbas mkurugenzi wa idara ya habari maelezo Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...