MKUU wa Mkoa wa Manyara Alexander Pastory Mnyeti amewafagilia wakuu wa Wilaya za Kiteto mhandisi Tumaini Magessa na Simanjiro mhandisi Zephania Chaula kuwa ndiyo wakuu wa wilaya bora kwa sasa kwenye mkoa wake, wenye kuchapa kazi na kuhudumia wananchi. 

Mnyeti akizungumza mjini Babati alisema mkuu wa wilaya ya Kiteto mhandisi Tumaini Magessa na mkuu wa wilaya ya Simanjiro mhandisi Zephania Chaula, ndiyo wakuu wa wilaya bora kwa sasa mkoani Manyara. 

Alisema anataja majina hayo mawili ya wakuu hao wa wilaya ili iwe changamoto kwa wakuu wengine wa wilaya za mkoa huo wenye wilaya tano, kutekeleza wajibu wao ipasavyo. Alisema wakuu wengine wa wilaya ambao hawajatajwa wasife moyo ila waongeze bidii na juhudi katika kuwatumikia wananchi na kutekeleza wajibu wao ipasavyo. 

Alisema anatangaza majina ya wakuu hao wa wilaya wanaongoza mkoani humo baada ya yeye kushauriana na Mwenyekiti wa CCM wa mkoa huo Simon Lulu na Katibu Tawala wa mkoa huo Missaile Mussa, ndipo wakapatikana hao. Alisema mkuu wa wilaya anapaswa kutoa maamuzi kwenye eneo lake la utawala na siyo kupiga simu kwa mkuu wa mkoa kila wakati kuomba msaada ili hali uwezo wa kutoa maamuzi anayo. 
Mkuu wa Wilaya ya Kiteto mhandisi Tumaini Magessa ambaye ametangazwa na Mkuu wa mkoa wa Manyara Alexander Mnyeti kuwa ndiyo anaongoza kwa uchapakazi.
Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro, mhandisi Zephania Chaula akisalimiana na wananchi wa eneo lake, mkuu wa mkoa wa Manyara Alexander Mnyeti amesema anashika nafasi ya pili kwa kuchapa kazi. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...