Naibu
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe .Constantine Kanyasu ametoa siku 30
kwa mkandarasi wa SUMA JKT, aliyepewa kazi ya kujenga jengo la ofisi
ya wizara hiyo katika mji wa serikali eneo la Ihumwa, Jijini Dodoma,
kuhakikisha jengo hilo linakamilika ndani ya siku hizo alizopewa
Amemshauri Mkandarasi huyo kufanya kazi usiku na mchana ili aweze kukamilisha ujenzi wa jengo hilo ndani ya siku hizo 30.
Amemshauri Mkandarasi huyo kufanya kazi usiku na mchana ili aweze kukamilisha ujenzi wa jengo hilo ndani ya siku hizo 30.
Ametoa rai hiyo mara baada ya kutembelea eneo hilo la ujenzi wa jengo la ofisi za Wizara hiyo linalotarajiwa kugharimu shilingi bilioni moja za kitanzania katika eneo la Ihumwa jijini Dodoma.
Aidha, Mhe.Kanyasu ameitaka kandarasi ya SUMA JKT ihakikishe inajenga jengo hilo kwa umakini, umahiri na viwango vya ubora wa hali ya juu vinavyokwenda sambamba na hadhi ya Wizara yenye mchango mkubwa kwenye pato la Taifa. Pia, Mhe.Kanyasu ameielekeza SUMA JKT wakati ikiendelea na maandalizi ya ujenzi wa jengo iwe inatoa taarifa kila siku kwa kila hatua inayofikia katika Ujenzi wa jengo hilo kwa Uongozi wa Wizara.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu akizungumza na baadhi ya Wakurugenzi wa Wizara hiyo mara baada ya kutembelea eneo ambalo jengo la ofisi ya Wizara ya Maliasili na Utalii litakapojengwa ndani ya siku 30 katika mji wa kiserikali wa Ihumwa jijini Dodoma kwa kandarasi ya SUMA JKT litakalogharimu bilioni moja.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu akipewa maelezo na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali watu wa Wizara hiyo, Bw. Lusius Mwenda mara baada ya kutembelea eneo ambalo jengo la ofisi ya Wizara ya Maliasili na Utalii litakapojengwa ndani ya siku 30 katika mji wa kiserikali wa Ihumwa jijini Dodoma kwa kandarasi ya SUMA JKT litakalogharimu bilioni moja.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu akioneshwa eneo na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali watu wa Wizara hiyo, Bw. Lusius Mwenda mara baada ya kutembelea eneo ambalo jengo la ofisi ya Wizara ya Maliasili na Utalii litakapojengwa ndani ya siku 30 katika mji wa kiserikali wa Ihumwa jijini Dodoma kwa kandarasi ya SUMA JKT litakalogharimu bilioni moja. (Picha zote na Lusungu Helel
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...