Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhandisi Stella Manyanya, akiwaonyesha mtambo maalum wa kuchemsha korosho wataalamu kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele. Wataalam hao wametembelea eneo la SIDO kujiridhisha kama linafaa kwa ajili ya kuanza kubangua korosho iliyonunuliwa na serikali.
Kaimu Meneja wa SIDO mkoa wa Mtwara, Zamla Dongwala, akimuonyesha mashine ya kukausha korosho Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji (hayupo pichani) wakati alipotembelea eneo la SIDO, mkoani Mtwara leo. Eneo hilo ni moja ya maeneo yaliyochaguliwa kuanza kutumiwa wa wabanguaji wa korosho wadogo kubangua korosho zilizonunuliwa na serikali.
Fundi umeme akiwa kwenye hatua za mwisho kukamilisha matengenezo ya mashine ya kuchambua korosho kama alivyokutwa na mpiga picha wetu eneo la SIDO mjini Mtwara leo. (Picha na Idara ya Habari-MAELEZO
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...