Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Ndugu Willam Erio na Mtendaji Mkuu wa TPB Ndugu Sabasaba Moshingi wamekutana leo jijini Dar es Salaam na kufanya mazungumzo ili kuendeleza mahusiano mazuri ya kibiashara kwa Taasisi zao.
Wakuu wa Taasisi hizo walikutana katika ofisi ya NSSF Makao Makuu na walizungumza mambo mbalimbali ikiwemo namna ya kuboresha mahusiano ya biashara baina ya Taasisi hizo mbili ambazo zimekuwa zikifanya huduma kwa muda mrefu.
Katika mazungumzo hayo Mkurugenzi mkuu wa NSSF Ndugu William Erio alimuahidi Mkurugenzi mtendji wa TPB aendelee kutarajia biashara yenye tija
Nae Mkurugenzi mkuu wa TPB Sebastia Moshingi amesema atawashawishi wastaafu wote wa NSSF waliokuwa wakilipwa pensheni zao kupitia Shirika la Posta wafungue Akaunti TPB ili waweze kufaidika na huduma mpya ya kulipa wastaafu wa NSSF ambapo mstaafu atalipwa pensheni yake moja kwa moja kwenye akaunti yake ya Benki hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Ndugu Willam Erio na Mtendaji Mkuu wa TPB Ndugu Sabasaba Moshingi wakiwa katika picha ya pamoja na kupeana mikono mara baada ya kumalizika kwa mazungumzo ya ushirikiano wa huduma baina ya Taasisi wanazoziongoza
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Ndugu Willam Erio na Mtendaji Mkuu wa TPB Ndugu Sabasaba Moshingi pamoja na watendaji wamashirika yote mawili wakiwa katika kikao cha kujadili huduma watakazoshirikiana.
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Ndugu Willam Erio na Mtendaji Mkuu wa TPB Ndugu Sabasaba Moshingi wakiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa mashirika wanayo yaongoza.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...