“Operesheni uvuvi haramu yapaisha mapato ya serikali kuu”

Operesheni za kudhibiti uvuvi haramu hapa nchini, zimeiwezesha serikali kuu kupata mrabaha wa Shilingi Bilioni 2.2 kuanzia Mwezi Desemba mwaka 2017 hadi Mwezi Novemba mwaka 2018, kutoka Shilingi Milioni 457.

Hayo yalibainishwa (01.12.2018) Jumamosi jijini Mwanza na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega wakati akiongoza kikao cha kufanya tathmini ya operesheni sangara kitaifa awamu ya tatu kwa mwaka 2018, kanda ya Ziwa Victoria, kikao kilichohudhuriwa na maafisa waliohusika katika operesheni hiyo, ambapo amesema kiasi hicho cha pesa kimeongezeka kutokana na mafanikio ya udhibiti wa mianya ya utoroshaji fedha.

“Mwaka 2017 mpaka tunafunga mwaka mwezi Desemba mrabaha wa serikali kuu kabla ya kufanya operesheni ulikuwa Shilingi Milioni 457, mwaka 2018 hadi Mwezi Novemba mrabaha wa serikali kuu ni Shilingi Bilioni 2.290, kutoka Shilingi Milioni 457 mpaka Shilingi Bilioni 2.290 unaweza kuona kwamba ni ongezeko la zaidi ya asilimia 200, hii maana yake kulikuwa na utoroshaji mkubwa wa fedha ambazo zingeingia katika mfumo mkuu wa serikali.” Alisema Mhe. Ulega.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega akitoa maelezo ya tathmini ya kitaifa ya operesheni sangara awamu ya III, mwaka 2018 kanda ya Ziwa Victoria kwa washiriki wa operesheni hiyo (hawapo pichani).
Afisa Mfawidhi kanda ya Ziwa Victoria Bw. Didas Mtambalike akisoma tathmini ya kitaifa ya operesheni sangara awamu ya III, mwaka 2018 katika kanda hiyo, kwa washiriki wa kikao kilichoongozwa na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega.

Baadhi ya washiriki wa operesheni sangara awamu ya III, mwaka 2018 wakifuatilia maelezo ya tathmini ya operesheni hiyo ilivyokuwa ikitolewa katika kikao hicho.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi washiriki wa operesheni sangara awamu ya III, Mwaka 2018 katika Kanda ya Ziwa Victoria


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...