Mkuu wa mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo amezitahadharisha kaya ambazo bado hazijaweza kurudi katika makazi yao kutokana na nyumba zao kuezuliwa na upepo na mvua kali na kuwafanya kuishi kwa mikusanyiko katika majengo ya serikali juu ya usafi wa mazingira ili kujiepusha na magonjwa ya mlipuko kutokana na uchache wa vyoo katika maeneo hayo.

Amesema kuwa ili kuhakikisha mlipuko huo hautokei ni vyema waathirika hao wakajibana kwa ndugu ambao nyumba zao hazikuathirka na kusisitiza kuwa kujisitiri katika majengo ya serikali ni kwa dharura tu huku wakiendelea kutafuta ufumbuzi wa misaada kwa wadau mbalimbali wa ndani nan je ya mkoa ili kuweza kuzisaidia familia hizo kurudi kwenye makazi yao ya kudumu.

“Tusingependa wandelee kukaa pale, kuna atahari nyingine ya magonjwa ya mlipuko kuwaweka watu zaidi ya 200 sehemu kama ile, miundombinu ya vyoo haitoshi, kwahiyo pale ni pa muda mfupi, jamani wale watu si wana ndugu? Hatuwezi kubanana banana huko, naiachia Halmashauri ndio maana nikasema Mkurugenzi ashuke huku ayaangalie yote haya,” Alisisitiza.
  Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo (katikati) pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dkt. Khalfan Haule (Kushoto) na Mkuu wa Shule ya Sekondari Kipeta Galus Gauwo (Kulia) wakitembelea moja ya mabweni ya Wasichana ya Sekondari ya kipeta yaliyoathiriwa na Mvua na Upepo mkali uliotokea usiku wa tarehe 8.12.2018. 
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo alipotembelea eneo la maafa yaliyosababisha kuharibiwa kwa nyumba 336 katika vijiji vya kilyamatundu na kipeta.
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo alipotembelea eneo la maafa yaliyosababisha kuharibiwa kwa nyumba 336 katika vijiji vya kilyamatundu na kipeta.
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo akikabidhi misaada kwa mwenyekiti wa kijiji cha Kipeta Leonard Ndenje wakati alipokwenda kutoa pole kwa waathirika hao hivi karibuni. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...