Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) linapenda kutoa taarifa kuwa kesho tarehe 09 Desemba, 2018litaadhimisha Sikukuu ya miaka 57 ya Uhuru wa Tanzania Bara kwa kufanya shughuli mbalimbali na kutoa huduma za Kijamii kwa Wananchi.

JWTZ litatoa huduma za tiba kwa kuwapima Wananchi magonjwa mbalimbali bila malipo.  Zoezi hilo la tiba litafanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam kesho Jumapili tarehe 09 Desemba 2018 kuanzia saa mbili (2.00) Asubuhi hadi saa nane (8.00) Mchana.

Wananchi wanataarifiwa kujitokeza ili kupima afya zao. Huduma za tiba zitakazotolewa ni pamoja na Ushauri Nasaha na Upimaji wa Virusi vya Ukimwi, Huduma za Mama na Mtoto, Upimaji wa Uzito, Shinikizo la Damu na Kisukari, Afya ya Kinywa na Meno pamoja na Uchangiaji wa Damu Salama.
 Aidha, kutakuwepo na “Press Conference” na Waandishi wa Habari katika viwanja hivyo kesho saa 4:00 Asubuhi.JWTZ linakialika chombo chako cha habari wakati wa “Press Conference” hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...