NaEmmanuel Masaka,Globu ya jamii

MAMLAKA ya Chakula na Dawa nchini Tanzania(TFDA) imefungua mafunzo ya wachunguzi wa maabara za dawa kwa nchi za Afrika jijini Dar es salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam katika Mkutano wa Kanda kwa nchi za Afrika, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Dk.Faustine Ndugulile ameeleza kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wachunguzi wa Maabara .

Dk.Ndugulile ameeleza kwa sasa duniani kumekuepo na usugu mkubwa  kwenye baadhi ya vyakula ambavo haviivi vizuri au  walaji wa nyama na mayai kutochunguza kwa makini kama kuna asilimia yoyote ambayo italeta madhara Kwenye miili yao pindi watakapokula vyakula ambavo si salama kwa afya zao.

Kwa upande wa Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya dawa na chakula ( TFDA)Adam Fimbo amefafanua zaidi kuwa lengo la mafunzo hayo si tu  kuwajengea uwezo wachunguzi wa maabara bali pia kutoa elimu kwa jamii jinsi gani wanatakiwa kuepuka vyakula ambavo vitaleta madhara baadae katika miili yao.

Fimbo amesema washiriki wa mafunzo hayo wapo 30 na nchi ambazo zinazoshiriki ni 22.Baadhi ya nchi hizo ni Algeria, Angola, Benin, Botswana, Burkina Faso, Burundi, Chad, DRC, Egypt, Kenya,Madagascar, Malawi, Mali, Mauritania, Morocco, Nigeria, SieraLeone, South Africa, Sudan, Uganda,  Tanzania na Zimbabwe.


Pia amewasisitiza  washiriki kuzingatia mafunzo hayo kwa ajili ya kunusuru na kupunguza kabisa uwezekano wa baadhi ya magonjwa ambayo si ya lazima endapo tutaweza kuyapatia ufumbuzi mapema .
Naibu waziri wa Afya maendeleo Jamii, jinsia, Wazee na Watoto Dk.Faustine Ndugulile akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo wachunguzi wa maabara za dawa kwa nchi za Africa, leo jijini Dar es Salaam.

Kaimu Mkurugenzi wa TFDA,Adam fimbo akizungumza na waandishi wa habari (hawapi pichani) leo jijini Dar es Salaam katika mafunzo ya kuwajengea uwezo wachunguzi wa maabara za dawa kwa nchi za africa.

Makamu Mkurugenzi wa Maabara kutoka Nigeria Dkt.Flosade Oluwabamieo akifafanua jambo mbele washiliki wa mafunzo ya wachunguzi wa maabara za dawa leo jijini Dar es Salaam.


Sehemu ya washiriki wakimzikiliza Naibu Waziri wa Afya Maendeo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dr. Faustine Ndungulile (hayupo pichani) alipokua akifungua mafunzo ya wachunguzi wa maabara za dawa kwa nchi za Africa, leo jijini Dar es Salaam.(picha na Emmanuel Massaka wa MMG)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...