Majengo yanayotumiwa na tume ya taifa ya uchaguzi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo yameshika moto na kuteketea mjini Kinsasa.

Moto huo ulizuka mwendo wa saa nane usiku wa manane na kuzua taharuki ikizingatiwa kwamba ni siku 10 zilizosalia kabla ya uchaguzi mkuu kufanyika nchini humo.

Moshi mweusi ulitanda angani na uliweza kuonekana kutoka mbali asubuhi kulipopambazuka, shirika la AFP limeripoti.

Moto huo unadaiwa kuathiri majengo ambayo yamekuwa yakitumiwa kuhifadhi vifaa vya uchaguzi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...