Hifadhi
ya Mazingira Asili ya Magamba iliyopo Lushoto, Tanga ni moja ya vivutio
vya hifadhi 12 za mazingira asilia vinavyosimamiwa na Wakala wa Huduma
za Misitu Tanzania (TFS).
Watu wengi wamekuwa wakisahau kuwa utalii wa ikolojia nao unafaida kwa
jamii yetu ili iweze kujifunza mambo mbali mbali kuhusu misitu na viumbe
hai.
Wakizungumza
kwa wakati tofauti mara baada ya kutembelea hifadhi ya mazingira ya
Magamba, Mfaume Salehe Msasa amesema “Kuwa Coordinator wa ni bahati
kwangu na furaha pia kwa kuwa nimejifunza vitu vingi sana tangia nimeaza
kuvolunteer @greathopetz pia naendelea kujifunza kwamaana kuwa
kujifunza hakunaga mwisho,"
Kwa kwaida kila mwaka @greathopetz hua tunatoa zawadi mbalimbali kwa
wanafunzi pamoja na shule zinazofanya miradi bora zaidi. Mwaka huu
tulikua na shule 100 ambazo zimefanya mradi na shule ambayo imefanya
mradi bora zaidi nakuweza kuwa mshindi wa kwanza ni Shule ya Sekondari
Zanaki.
“Miradi
ya mwaka huu imekua ni ya tofauti kubwa kwa mshindi wa mradi wa Uwezo
Award kupata zawadi nyingi na wamepewa safari ya kitalii ya kwenda msitu
wa Magamba kwa kudhaminiwa na Wakala wa huduma za misitu Tanzania na
Bodi ya Utalii Tanzania (TTB).
Nae Meneja wa Wakala wa huduma za misitu Tanzania (TFS) ameshukuru jinsi wanafunzi walikuwa na moyo wa kujifunza kuhusu mazingira na kuomba shule pamoja na wazazi waweze kujitokeza kuwapeleka watoto wao katika vivutio mbali mbali vya utalii wa ikolojia ambao watu wengi wamekuwa wakiusahau.
Nae Meneja wa Wakala wa huduma za misitu Tanzania (TFS) ameshukuru jinsi wanafunzi walikuwa na moyo wa kujifunza kuhusu mazingira na kuomba shule pamoja na wazazi waweze kujitokeza kuwapeleka watoto wao katika vivutio mbali mbali vya utalii wa ikolojia ambao watu wengi wamekuwa wakiusahau.
Afisa Utalii wa Hifadhi ya Mazingira Asili ya Magamba iliyopo Lushoto, Tanga Samiji Mlemba (katikati) akitoa maelezo kwa wanafunzi wa Sekondari ya Zanaki jijini Dar es Salaam waliopata ufadhili wa kutembelea hifadhi hiyo waliopewa na Wakala wa huduma za misitu Tanzania (TFS) na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) kupitia mradi wa Uwezo Award uliendeshwa na Shirika lisilo la kiserikali la Great Hope Foundation. Picha zote na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG - Lushoto.
Afisa Utalii wa Hifadhi ya Mazingira Asili ya Magamba iliyopo Lushoto, Tanga Samiji Mlemba akiwa ameongozana na kuwapa maelezo wanafunzi na wanahabari waliokuwa katika ziara hiyo.
Afisa Utalii wa Hifadhi ya Mazingira Asili ya Magamba iliyopo Lushoto, Tanga Samiji Mlemba akitoa maelezo machache wakati wanafunzi hao walipofika kituo cha Mshai wakielekea katika kilele cha mlima Kigulu Hakwewa.
Wanafunzi wakifurahia katika mlango wa pango la Wajerumani walilolitumia katika vita vya kwanza vya dunia vilivyotokea mwaka 1914 - 1918.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...