Na John Nditi, Morogoro
NAIBU
waziri wa Ujenzi , Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi, Atashasta Nditiye
ameiagiza Baraza la Wafanyakazi la Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL)
pamoja na Menejimenti ya Kampuni kuimarisha kitengo cha masoko na
kufanya ufuatiliaji kwa watumishi na mawakala wanaoihujumu Kampuni
hiyo.
Naibu
Waziri alisema hayo katika hotuba yake ya ufunguzi wa kikao cha tatu
cha baraza la wafanyakazi wa ATCL lililofanyika mjini Morogoro.
Alisema
, kwa muda mrefu kumekuwa na manenoo mengi yanayosemwa juu ya kuwepo
hujuma dhidi ya Ndege za ATCL hasa kwenye njia ya Kilimanjaro na
Mbeya .Mbali
na njia hizo pia huduma hizo zinafanywa kwa maeneo mengine ambapo
wateja wanapohitaji huduma za ATCL huambiwa kuwa ndege zimejaa wakati
jambo hilo si kweli na matokeo yake ndege zinaondoka bila kujaa abiria.
“
Baadhi ya makawala wanaouza tiketi za ATCL wanaonwa na makampuni
mengine ya Ndege ili wajaze kwanza ndege zao kwa kutoa maelezo kwa
wateja wanaohitaji kusafiri na ndege zetu za umma kuwa zimejaa , lakini
baadaye zinaondoka bila kujaa abiria” alisema Naibu Waziri Nditiye.
Naibu
Waziri huyo alisema “ Huduma za ndege zetu ni nzuri na nauli yake ni
ndogo na pia ndege zetu zote ni mpya lakini hazijai tofauti na za
makampuni binafsi ambayo bei zake ni za juu na huduma zao hazifanani na
za ATCL “ alisema Naibu Waziri Nditiye .
Naibu
waziri wa Ujenzi , Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi, Atashasta Nditiye (
kushoto) akijadiliana jambo na Mkurugenzi mkuu wa ATCL, Ladislaus
Matindi ( wa pili kushoto ) baada ya Naibu Waziri kufungua kikao cha
tatu cha baraza la wafanyakazi wa ATCL lililofanyika mjini Morogoro.
Naibu
waziri wa Ujenzi , Uchukuzi na Mawasiliano , Mhandisi Atashasta Nditiye
( kulia ) akijadiliana jambo na Mkurugenzi mkuu wa ATCL, Ladislaus
Matindi ( kushoto ) kwa ajili ya kufungua kikao cha tatu cha baraza
la wafanyakazi wa ATCL kilichofanyika mjini Morogoro.
Baadhi
ya wajumbe wa Baraza la wafanyakazi wa ATCL wakimsilikiza Naibu waziri
wa Ujenzi , Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi, Atashasta Nditiye (
hayupo pichani ) alipofungua kikao cha tatu cha baraza hilo mjini
Morogoro.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...