*Awataka waliopewa dhamana wazingatie viwango vya kimataifa
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amezinduaChaneli ya Taifa ya Utalii iitwayo Tanzania Safari Channel na amewataka watu wote waliopewa dhamana ya kuiendesha wahakikishe wanazingatia viwango vya kimataifa katika vipindi watakavyokuwa wanaviandaa. “Vipindi vyenu ni lazima vivutie kama vile tunavyoviangalia katika chaneli za wanyama za kimataifa kama vile National Geographic, Discovery, Travel na zingine ili lengo lililokusudiwa wakati wa kuanzishwa kwake litime.”

Ameyasema hayo leo (Jumamosi, Desemba 15) wakati akizindua chaneli hiyo kwenye Ofisi za TBC, Mikocheni, jijini Dar es Salaam, ambapo ametoa wito kwa Wizara zote zinazohusika na uanzishwaji wa Chaneli hiyo kuhakikisha zinailea wakati ikijijenga kujiendesha kibiashara.

Amesema Tanzania ni moja ya nchi duniani zilizotenga moja ya tatu ya eneo lote la nchi kwa ajili ya uhifadhi, ambapo kuna tamaduni za makabila mbalimbali, ngoma za kuvutia, vyakula vya asili, sinema za maisha yetu na lugha adhimu ya Kiswahili.

“Hivyo, kwa kuanzishwa kwa chaneli hii inayotengeneza vipindi na kuonesha vivutio hivi ndani na nje ya Tanzania itasaidia watalii huko waliko kujua huu utajiri wetu na kuchagua kuja kutalii nchini. Ni matumaini yangu kuwa hii Tanzania Safari Channel ninayoizindua leo itaongeza thamani katika kuvutia watalii wengi zaidi kutembelea Tanzania.”

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua Chaneli ya Tanzania Safari Channel kwenye  Viwanja vya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) jijini Dar es salaam Desemba 15, 2018.  Kushoto ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe na kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Dkt. Ayoub Ryoba. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua Chaneli ya Tanzania Safari Channel kwenye  Viwanja vya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) jijini Dar es salaam Desemba 15, 2018.  Kushoto ni Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe, wapili kulia ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla na kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Dkt. Ayoub Ryoba. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Ufundi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Upendo Mbele wakati alipotembelea Studio mpya za TBC kabla ya kuzindua chaneli ya Tanzania Safari Channel, Desemba 15, 2018. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa TBC,  Dkt. Ayoub Ryoba.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipozindua Chaneli ya  Tanzania Safari Channel kwenye viwanja vya Ofisi za Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Mikocheni jijini Der es slaaam, Desemba 15, 2018. 
 Baadhi ya viongozi na wageni waalikwa wakimsikiliza Waziri Mkuu,  Kassim Majaliwa wakati alipozindua Chaneli ya Tanzania Safari Channel kwenye viwanja vya Ofisi za Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) jijini Dar es salaam, Desemba 15, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) baada ya kuzindua Chaneli ya Tanzania Safari Chanmnel Kwenye viwanja vya TBC,  Mikocheni jijini Dar es salam, Desemba 15, 2018. (Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...