Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Cornel Muro  ameendelea kuungwa mkono na wadau wa Maendeleo Kwa kukabidhiwa awamu ya kwanza ya Mifuko 100 ya Saruji kutoka katika Kampuni ya Farm Acces Ltd kwa ajili ya kuunga mkono jitihada za ujenzi wa vyumba vya madarasa zaidi 100 Arumeru.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa saruji hiyo Ndugu Muro mbali na kushukuru Kwa msaada huo , amepongeza jitihada zinazofanywa na  kampuni hiyo ambayo bado haijaanza uzalisha wa Dawa za mifugo lakini wameweza kuchangia mifuko 100 Kwa awamu ya kwanza na kuwataka wadau wengine kuunga mkono juhudi Za ujenzi wa vyumba vya madarasa .

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Dkt. Saimoni amepongeza juhudi zinazofanywa  Mkuu wa Wilaya ya Arumeru chini ya serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe. Rais John Pombe Magufuli na kusisitiza kutoa msaada zaidi pindi watakapoanza uzalishaji kiwandani hapo.

Wadau hao wa maendeleo Waliahidi kuchangia mifuko 200 ya Saruji na kwa Awamu ya kwanza wamemkabidhi Dc Muro mifuko 100 ya saruji na kuahaidi ndani ya muda mfupi watamkabidhi tena Mkuu wa Wilaya mifuko 100 mingine iliyobakia.

Dc Muro anaendelea na ziara yake ya kuhamasisha, na kusimamia ujenzi wa vyumba vya madarasa vya shule mbalimbali Za sekondari katika Wilaya ya Arumeru Kwa lengo la kumaliza changamoto ya madarasa kuanzia shule Za msingi, sekondari na kidato Cha tano na sita .
 Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Cornel Muro  ameendelea kuungwa mkono na wadau wa Maendeleo Kwa kukabidhiwa awamu ya kwanza ya Mifuko 100 ya Saruji kutoka katika Kampuni ya Farm Acces Ltd kwa ajili ya kuunga mkono jitihada za ujenzi wa vyumba vya madarasa zaidi 100 Arumeru.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...