Na Mwandishi Wetu Mbinga
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile ameitaka jamii kuwawezesha watoto wa kike kupata elimu ili kuwa na Jamii yenye mabinti wasomi na kuondokana na ukandamizaji wa watoto wa kike na wanawake.
Dkt. Ndugulile ametoa rai hiyo wilayani Mbinga mkoani Ruvuma wakati akishirikiana na wananchi katika ujenzi wa Bweni la shule ya Sekondari Mikalanga ambalo kwa kiasi kikubwa wananchi wametoa nguvu zao katika kufanikisha ujenzi huo.
Dkt. Ndugulile amesisitiza kuwa suala la elimu kwa mtoto wa kike na muhimu kutokana na changamoto za mtoto wa kike hasa suala la mimba za utotoni ambazo zinapelekea kupotea kwa ndoto za wanafunzi wa kike wengi.
Naibu Waziri Ndugulile amesema kuwa kwa mujibu wa takwimu zilizopo Mtoto mmoja kati ya watoto watatu wa kike hupata mimba za utotoni na kukatisha ndoto za Mtoto wa kike kupata elimu kati ya miaka 15 mpaka 19 ikiwa sawa na asilima 27.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.
Dkt. Faustine Ndugulile akiwasili katika shule ya Sekondari Mikalanga
akiongozana na Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Mhe. Cosmas Nshenye na Mbunge wa
Viti Maalum kwa mkoa wa Ruvuma Mhe. Jacquiline Ngonyani kwenda
kushirikiana na wananchi katika ujenzi wa bweni la wasichana shuleni
hapo.
Naibu
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt.
Faustine Ndugulile akiangalia kikundi cha ngoma za asili katika shule
ya Sekondari Mikalanga akiongozana na Mkuu wa Wilaya ya Mbinga
Mhe.Cosmas Nshenye na Mbunge wa Viti Maalum kwa mkoa wa Ruvuma Mhe.
Jacquiline Ngonyani kwenda kushirikiana na wanachi katika ujenzi wa
bweni la wasichana shuleni hapo.
Naibu
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt.
Faustine Ndugulile akishirikiana na Mbunge wa Viti Maalum kwa mkoa wa
Ruvuma Mhe. Jacquiline Ngonyani katika ujenzi wa bweni la wasichana
katika Shule ya Sekondari Mikalanga.
Naibu
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt.
Faustine Ndugulile akizungumza na wananchi waliojitokeza kushirki katika
ujenzi wa bweni la wasichana katika shule ya Sekondari Mikalanga ikiwa
ni juhudi za wananchi kupunguza adha ya watoto wa kike kupata mimba
shuleni.
Naibu
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt.
Faustine Ndugulile akikabidhi mmoja ya mifuko 50 aliyochangia katika
ujenzi wa bweni la wasichana katika shule ya sekondari Mikalanga ikiwa
ni juhudi za wananchi kupunguza adha ya watoto wa kike kupata mimba
shuleni.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...