Na Editha Karlo wa blog ya jamii,Kigoma.

KAMATI ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya Kibondo wamekamata nguo zinazofanana na za sare za kijeshi katika makambi ya wakimbizi.

Akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake pamoja na kamati ya ulinzi ya usalama ya Mkoa, Kaimu Mkuu wa  Mkoa wa Kigoma Samson Hanga alisema kuwa nguo hizo zilikamatwa tarehe 31 mwezi wa 12 mwaka jana majira ya kati  saa tano asubuhi hadi sita mchana kwenye kwenye makambi ya wakimbizi.

Hanga alisema kuwa jumla ya nguo zinazofanana na sare za kijeshi 1947 zilikamatwa katika kambi ya wakimbizi ya Mtendeli na Nduta zilizopo Mkoani Kigoma.

"Kambi ya wakimbizi ya nduta zilikamatwa nguo 1325 na kambi ya wakimbizi ya mtendeli pia zilikamatwa nguo 1325"alisema

Alisema uchunguzi wa tukio hilo unaendelea ili  kuwabaini waliongiza sare hizo na lengo lao.



 Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Samson Hanga akiongea na waandishi wa habari kuhusu kukamatwa kwa lundo la nguo zinazofanana na sare za kijeshi katika makambi ya wakimbizi Wilayani Kibondo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...