Rais
wa mtandao wa wasanii wa Injili na Maadili Dkt. Godwin Maimu
akizungumza katika Tamasha hilo lililofanyika Buza Jijini Dar es salaam Buza Kipera
Picha
ya Viongozi wa Mtandao wa wasanii wa Injili na maadili wa pili kutoka
kulua ni Rais wa Tagoane Taifa Dkt. Godwin Maimu, aliyrpo kushoto kwake
ni Katibu mkuu Mchungaji Lucy, wa kwanza kushoto ni Katibu mkuu mwenza
Silvanus Mumba akifuatiwa na Makamu wa Rais Tagoane, Florah Sungura.
Mchungaji mwenyeji Tamasha lilipofanyika Apostal Israel Popapo kutoka Jijini Dar es salaam, katika kanisa la ETERNITY GOSPEL CHURCH, Buza Kipera
Uimbaji ukiendelea kama inavyoonekana katika picha kafika kanisa la ETERNITY GOSPEL CHURCH Buza Kipera
Picha ya pamoja ya wasanii mbalimbali wa Injili waluohudhuria katika tamadha hilo lililopewa jina la Madhabahu ya shukrani
NA.VERO IGNATUS
Mtandao
wa wasanii wa Injili na maadili Nchini(Tagoane) wanafanya Tamasha leo
la kutoa shukrani kwa Mungu kwa kuwapa ulinzi na Kibali tangia
kuanzishiswa kwa mtandao huo
Akizungumza katibu mkuu mtendaji Tagoane Taifa Silvanus Mumba amesema kuwa Tamasha hilo wamelipa jina la Tukuza Festival Madhabahu ya shukrani ambapo wananzia Jijini Dar es salaam ndipo wataelekea mikoa mingine
Amesema
lengo kuu ni kumshukuru Mungu kwa matendo makuu aliyowatendea tangia
kuanzishwa kwa mtandao huo sambamba na mafanikio yaliyopatikana ya
kuwaleta waimbaji wa pamoja.
Silvanus
amesema kuwa hadi sasa wamekuwa na Mafanikio Makubwa tangia kuanzishwa
kwa TAGOANE, wameweza kusaidia Watoto Yatima, wameutangaza Utalii wa
ndani wameweza kusaidia Vifaa vya matibabu katika Hospitali Mount Meru
sambamba na kusaidia Vijana Elimu juu ya ujasiliamali,
Akielezea matazamio waliyonayo ni kuweza kuwasaidia wasanii Kuwa na UCHUMI imara kupitia Mfuko wa TAGOANE LOAN FUND, Kuwa na Wasanii walio Tayari kujito kwaajili ya Jamii na makundi Maalumu Kama Wazee, Yatima, wajane, vilema, na Wagonjwa
Amesema
kuwa wanaendelea Kuwa na Utaratibu wa Kuibua vipaji Mashuleni kwa
Kushirikiana na Taasisi ya waalimu wa shule BinafsiTanzania (TPTU)
Lakini pia Kujiunganisha na wadau wa Maendeleo Kama SIHAONE TUNAPENDANA
Ltd
Tunapenda
kuwaambia Wasanii wote, wakristo walio Kwenye sekta ya Sana, kujiunga
na TAGOANE kwasababu ndio Pahala sahihi amvako wataweza kujiweka Akiba
na kukopa inapohitajika, Kupata Fursa ya Mafunzo ya ujasiliamali na
Sheria ya hatimiliki, Elimu juu ya Ubunifu Lakini pia Watajitolea kwa
jamii pia ifaidike kupitia yeye
Mikoa
mingine ambayo wanatazamia kufanya Tamasha hilo ni pamoja na Dodoma,
Morogoro, kwa sasa wameanza na Jiji la Dar es salaam mikoa mingine
wataendelea kutoa taarifa , lengo kuu ni Kumpelekea Mungu Shukurani za
pekee kwa Kuisimamisha Tagoane Kuwa ya Mfano.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...