Rais wa mtandao wa wasanii wa Injili na Maadili Dkt. Godwin Maimu akizungumza katika Tamasha hilo lililofanyika Buza Jijini Dar es salaam Buza Kipera
 Picha ya Viongozi wa Mtandao wa wasanii wa Injili na maadili wa pili kutoka kulua ni Rais wa Tagoane Taifa Dkt. Godwin Maimu, aliyrpo kushoto kwake ni Katibu mkuu Mchungaji Lucy, wa kwanza kushoto ni Katibu mkuu mwenza Silvanus Mumba akifuatiwa na Makamu wa Rais Tagoane, Florah Sungura. 
 Mchungaji mwenyeji Tamasha lilipofanyika Apostal Israel Popapo kutoka  Jijini Dar es salaam, katika  kanisa la ETERNITY GOSPEL CHURCH, Buza Kipera
 Uimbaji ukiendelea kama inavyoonekana katika picha kafika kanisa la ETERNITY GOSPEL CHURCH Buza Kipera
 Picha ya pamoja ya wasanii mbalimbali wa Injili waluohudhuria katika tamadha hilo lililopewa jina la Madhabahu ya shukrani


NA.VERO IGNATUS

Mtandao wa wasanii wa Injili na maadili Nchini(Tagoane) wanafanya Tamasha leo la kutoa shukrani kwa Mungu kwa kuwapa ulinzi na Kibali tangia kuanzishiswa kwa mtandao huo

Akizungumza  katibu mkuu mtendaji  Tagoane Taifa Silvanus Mumba amesema kuwa Tamasha hilo wamelipa jina la Tukuza Festival Madhabahu ya shukrani ambapo wananzia Jijini Dar es salaam ndipo wataelekea mikoa mingine

Amesema lengo kuu ni kumshukuru Mungu kwa matendo makuu aliyowatendea tangia kuanzishwa kwa mtandao huo sambamba na mafanikio yaliyopatikana ya kuwaleta waimbaji wa pamoja.

Silvanus amesema kuwa hadi sasa wamekuwa na  Mafanikio Makubwa tangia kuanzishwa kwa TAGOANE, wameweza kusaidia Watoto Yatima, wameutangaza Utalii wa ndani wameweza kusaidia Vifaa vya matibabu katika  Hospitali Mount Meru sambamba na kusaidia Vijana Elimu juu ya ujasiliamali,

Akielezea matazamio waliyonayo ni  kuweza kuwasaidia wasanii Kuwa na UCHUMI imara kupitia Mfuko wa TAGOANE LOAN FUND, Kuwa na Wasanii walio Tayari kujito kwaajili ya Jamii na makundi Maalumu Kama Wazee, Yatima, wajane, vilema, na Wagonjwa

Amesema kuwa  wanaendelea Kuwa na Utaratibu wa Kuibua vipaji Mashuleni kwa Kushirikiana na Taasisi ya waalimu wa shule BinafsiTanzania (TPTU) Lakini pia Kujiunganisha na wadau wa Maendeleo Kama SIHAONE TUNAPENDANA Ltd

Tunapenda kuwaambia Wasanii wote, wakristo walio Kwenye sekta ya Sana, kujiunga na TAGOANE kwasababu ndio Pahala sahihi amvako wataweza kujiweka Akiba na kukopa inapohitajika, Kupata Fursa ya Mafunzo ya ujasiliamali na Sheria ya hatimiliki, Elimu juu ya Ubunifu Lakini pia Watajitolea kwa jamii pia ifaidike kupitia yeye

Mikoa mingine ambayo wanatazamia kufanya Tamasha hilo ni pamoja na Dodoma, Morogoro, kwa sasa wameanza na Jiji la Dar es salaam mikoa mingine wataendelea kutoa taarifa ,  lengo kuu ni Kumpelekea Mungu Shukurani za pekee kwa Kuisimamisha Tagoane Kuwa ya Mfano. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...