Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Prof. Dos Santos Silayo ambaye ndiye mwenyekiti wa Baraza la Saba la Wafanyakazi TFS akijadiliana jambo na katibu wa baraza hilo Ibrahim Mwanga muda mfupi baada ya kufungua kikao hicho cha siku mbili (Januari 10 - 11, 2019) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha mapema hivi leo. Hata hivyo mwenyekiti huyo aliwaeleza wajumbe kuwa kikao hicho kitafunguliwa rasmi kesho na mgeni rasmi wa mkutano huo Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Prof. Adolf Mkenda baada ya kupatwa na dharula leo.
Baadhi ya wajumbe wa mkutano huo wakiwa wameshikana mikono huku wakiimba wimbo wa kuhamasisha mshikamano miongoni mwa wafanyakazi kama sehemu ya ufunguzi wa kikao hicho.
...baadhi ya wajumbe wakisikiliza mada ya uanzishwaji wa Chama cha Kuweka na Kukopa cha Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS SACCOS) iliyotolewa na Mwakilishi wa Chama cha Ushirika kutoka Wilaya ya Temeke, Dorina Mwanri (hayupo pichani) ambapo aliwataka viongozi wa muda walioteuliwa kuhakikisha wanazunguka kutoa elimu ya kutosha kwa wafanyakazai ili waweze kujiunga na chama hicho. TFS SACCOS imeanzishwa Disemba 2018.
Baadhi ya Wajumbe wa Mkutano wa Saba wa Baraza la Wafanyakazi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania wakijadiliana jambo kutoka kwenye bango kitita la mkutano huo.
Wajumbe wakifuatilia mkutano huo




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...