Mfuko wa Rais wa Kujitegemea (PTF) umepongezwa kwa utekelezaji mzuri wa Sera ya Uchumi wa Viwanda inayohimizwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa kutoa mikopo kwa makundi maalumu ya watu wenye ulemavu, akina mama na vijana wanaojihusisha na shughuli za ujasiriamali jijini Dar es Salaam.
Pongezi hizo zimetolewa na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) wakati wa ziara ya kikazi ya kuwatembelea watumishi wa Mfuko wa Rais wa Kujitegemea kwa lengo la kufahamu majukumu ya mfuko huo na kuhimiza uwajibikaji, ambapo alipata fursa ya kujionea wanufaika wa mikopo inayotolewa na mfuko huo.
Mhe. Dkt. Mwanjelwa amesema kuwa, makundi yaliyopatiwa mikopo ambayo ni kundi maalumu la walemavu la Furaha ya Wanawake Wajasiriamali Viziwi Tanzania (FUWAVITA), kikundi cha UWAZI SHALOOM cha akina mama wasindikaji, Kikundi cha MAKINI FOOD SUPPLIES cha akina mama wasindikaji na kikundi cha MAB cha vijana ni mfano mzuri wa kuigwa kwa kutekeleza sera ya Uchumi wa viwanda kwa vitendo kwani wanazalisha bidhaa zenye ubora ambazo ni mvinyo, viungo vya mchuzi, viungo vya chai, siagi ya karanga, mango pickle na mabeji ya wanafunzi wa shule za awali, za msingi na vyuo.
Naibu
Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akizungumza na watumishi wa Mfuko wa Rais
wa Kujitegemea (PTF) wakati wa ziara ya kikazi alipowatembelea ofisini
kwao jijini Dar es Salaam kwa lengo la kufahamu majukumu ya mfuko na
kuhimiza uwajibikaji, ambapo pia alipata fursa ya kujionea wanufaika wa
mikopo inayotolewa na mfuko huo.
Naibu
Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akikabidhiwa nyaraka mbalimbali na
Mkurugenzi wa Mfuko wa Rais wa Kujitegemea (PTF) Bi. Haigath Kitala mara
baada ya mkurugenzi huyo kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wakati wa
ziara ya kikazi ya Dkt. Mwanjelwa katika ofisi za PTF jijini Dar es
Salaam, ziara ilikuwa na lengo la kufahamu majukumu ya mfuko na
kuhimiza uwajibikaji.
Naibu
Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akisikiliza maelezo ya Bi. Rose Kalulika
kuhusu bidhaa zinazozalishwa na kikundi cha akina mama cha UWAZI
SHALOOM wakati wa ziara ya kikazi katika ofisi za PTF jijini Dar es
Salaam, ambapo alipata fursa ya kuzungumza na wanufaika hao wa mikopo
inayotolewa na PTF.
Naibu
Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akishuhudia bidhaa zinazotengenezwa na
kikundi cha Furaha ya Wanawake Wajasiriamali Viziwi Tanzania
(FUWAVITA), kikundi cha UWAZI SHALOOM cha akina mama wasindikaji,
Kikundi cha MAKINI FOOD SUPPLIES cha akina mama wasindikaji na kikundi
cha MAB cha vijana wakati wa ziara yake ya kikazi katika ofisi za PTF
jijini Dar es Salaam, ambapo alipata fursa ya kuzungumza na wanufaika
hao wa mikopo inayotolewa na PTF.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...