Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda
Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amewaalika Wananchi Wapenda maendeleo kuungana na Rais Dkt. John Magufuli kwenye mapokezi ya Ndege ya Sita ya Serikali aina ya Airbus A220-300 itakayowasili Nchini Kesho January 11 Saa sita Mchana ikitokea Nchini Canada.
Hafla ya mapokezi ya ndege hiyo itafanyika kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere jijini Dar es salaam.
Makonda amesema kuwa anatumaini wananchi wengi watajitokeza katika kuunga mkono jitihada za Mh. Rais ambaye amekuwa mstari wa mbele katika kuleta maendeleo.
Rais Magufuli aliahidi na sasa anatekeleza.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...