Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
 
SHIRIKA la Umeme Tanzania(TANESCO) Mkoa wa Arusha limesema kwa kushirikiana na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Jery Murro wamefanikiwa kudhibiti vishoka na wahujumu wa miundombinu ya shirika hilo.

Hayo yameelezwa na Meneja wa TANESCO Mkoa wa Arusha Mhandisi Herini Mhina wakati anazungumzia hatua ambazo zimefanyika katika kukabiliana na vishoka pamoja na wahujumu wa miundombinu.

Kuhusu vishoka amesema TANESCO wamekuwa wakichukua hatua mbalimbali kukabiliana na vishoka na baadhi ya hatua hizo kwa wale ambao wanabainika wanachukuliwa hatua.Pia wamekiwa wakiondoa miundombinu ya umeme ambayo imewekwa na vishoka.

"Maeneo ya USA tuling'oa nguzo ambazo ziliwekwa na vishoka,pia tumekuwa tukiondoa hata LUKU ambazo tunabaini zimewekwa na hao vishoka.Tumechukua mbalimbali ikiwamo ya wanaobainika kuchukuliwa hatua ya kupelekwa Polisi sheria ichukue mkondo wake.Tumefanikiwa sana kuwadhibiti vishoka kwani TANESCO tupo makini .

" Tunashirikiana kwa karibu na Mkuu wa Wilaya Murro,kila tunapomueleza katika hili anatoa ushirikiana na kwenye matukio mengi yanayohusu kukamata vishoka au wanaohujumu miundombinu amekuwa pamoja nasi,"amefafanua Mhandisi Mhina.

Kwanini Murro amekuwa akishiriki kwa karibu kukomesha vishoka,Meneja Mhina amejibu kuwa katika Wilaya ya Arumeru tatizo la vishoka na wanaohujumu moundombinu lilikuwa kubwa na katika kulishughulikia walimpa taarifa Mkuu huyo wa Wilaya na tangu alipofika wanashirikiana sana.

Ameongeza katika hujuma ya miundomboni nayo wamefanikiwa na wanaendelea kufuatilia hatua kwa hatua ili kuwabaini wenye kuiharibu miundomboni."Kuna watu wanaiba waya wa mita 10,sasa hiyo ni hujuma ya miundombinu ya umeme."

Kwa upande wake  Menaja Mwandamizi wa Miradi TANESCO Mhandisi Emmanuel Manirabona amezungumzia mikakati ya shirika hilo la kudhibiti vishoka ambapo amefafanua moja ya mkakati ni kuhakikisha vifaa vyote vya shirika hilo vinabaki kuwa mali ya shirika.

Amesema hivyo hata mfanyakazi au mtumishi yoyote wa TANESCO ataruhusiwa kutumia mali ya shirika hilo akiwa mfanyakazi na baada ya hapo hataruhusiwa.

"Ukifuatilia utaona matangazo pale inapotokea kuna mfanyakazi wetu ameondolewa TANESCO na wakati mwingine tunasema kuwa mtu fulani si mfanyakazi wetu na hatutahusika na chochote ambacho atakifanya,"amesema Mhandisi Manirabona.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...