Wadau mbalimbali wa maendeleo Wilayani Arumeru wameendelea Kujitokeza na kumuunga mkono Mkuu wa Wilaya hiyo Ndugu Jerry Cornel Muro katika ujenzi wa madarasa.

Wadau hao wa maendeleo Waliahidi kuchangia mifuko 100 ya Saruji na kwa Awamu ya kwanza leo Hii wamemkabidhi Dc Muro mifuko 50 ya saruji na kuahaidi ndani ya wiki mbili zijazo watakamilisha ahadi yao. 

Wakizungumza mara baada ya kukabidhi mifuko hiyo ya saruji wameeleza kuwa Lengo la kumuunga mkono Dc Muro katika ujenzi wa madarasa ni kwamba wanaamini Katika kujenga jamii imara lazima kuhakikisha Elimu inapewa kipaumbele cha pekee pia wameeleza hawana budi kuunga mkono juhudi za serikali ya Awamu ya tano chini ya Rais wetu mpendwa Dr. John Pombe Joseph Magufuli.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Arumeru amewashuku wadau hao wa maendeleo kuendelea kujitolea katika kuhakikisha wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza wanapata madarasa ya kutosha

Pia Dc Muro amewaomba Wadau wengine kuja kumuunga mkono katika kuchangia ujenzi wa madarasa katika Halmashauri ya Arusha Dc na Halmashauri ya Meru. 

Imetolewa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Arumeru
20/01/2019

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...